< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
Et les enfants d'Israël, selon leur nombre, les chefs de famille, les chefs de milliers et de centaines, et les officiers qui étaient au service du roi dans les divisions qui entraient et sortaient chaque mois, pendant tous les mois de l'année, étaient au nombre de vingt-quatre mille.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
A la tête de la première division, pour le premier mois, était Jashobeam, fils de Zabdiel. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
Il était des fils de Pérets, chef de tous les chefs de l'armée pour le premier mois.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le chef de la division du second mois était Dodaï, l'Ahochite, et sa division, et Mikloth, le chef; sa division comptait vingt-quatre mille hommes.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
Le troisième chef de l'armée, pour le troisième mois, était Benaja, fils de Jehojada, le souverain sacrificateur. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
C'est ce Benaja qui était le plus fort parmi les trente et au-dessus des trente. Il avait pour division Ammizabad, son fils.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le quatrième chef, pour le quatrième mois, était Asaël, frère de Joab, et Zebadia, son fils, après lui. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le cinquième commandant, pour le cinquième mois, était Schamhuth, le Jizrachite. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le sixième commandant, pour le sixième mois, était Ira, fils d'Ikkesh, le Tekoïte. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le septième commandant, pour le septième mois, était Hélez, le Pelonite, des fils d'Éphraïm. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le huitième, pour le huitième mois, était Sibbecaï, le Hushathite, des Zérachites. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le neuvième, pour le neuvième mois, était Abiézer, l'Anathothite, des Benjamites. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le dixième chef, pour le dixième mois, était Maharaï, le Nethophathite, des Zérachites. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le onzième, pour le onzième mois, était Benaja, de Pirathon, des fils d'Éphraïm. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Le douzième chef, pour le douzième mois, était Heldaï, de Netophath, d'Othniel. Il avait une division de vingt-quatre mille hommes.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
De plus, sur les tribus d'Israël pour les Rubénites: Eliezer, fils de Zicri; pour les Siméonites: Schephatia, fils de Maaca;
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
pour les Lévites: Haschabia, fils de Kemuel; pour Aaron: Tsadok;
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
pour Juda: Elihu, l'un des frères de David; pour Issachar: Omri, fils de Micaël;
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
pour Zabulon: Ismaeja, fils d'Obadia; de Nephthali, Jeremoth, fils d'Azriel;
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
des fils d'Ephraïm, Hoshea, fils d'Azazia; de la demi-tribu de Manassé, Joël, fils de Pedaja;
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
de la demi-tribu de Manassé en Galaad, Iddo, fils de Zacharie; de Benjamin, Jaasiel, fils d'Abner;
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
de Dan, Azarel, fils de Jerocham. Tels étaient les chefs des tribus d'Israël.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
Mais David ne fit pas le décompte de ceux qui étaient âgés de vingt ans et moins, car Yahvé avait dit qu'il multiplierait Israël comme les étoiles du ciel.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Joab, fils de Tseruja, commença à faire le recensement, mais il ne le termina pas, et la colère s'abattit sur Israël à cause de cela. Le nombre n'a pas été mis en compte dans les chroniques du roi David.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Azmaveth, fils d'Adiel, était responsable des trésors du roi. Jonathan, fils d'Ozias, était chargé des trésors des champs, des villes, des villages et des tours.
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
Ezri, fils de Chelub, était chargé des travaux des champs pour le labourage du sol.
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
Sur les vignes, Shimei, le Ramathite. Zabdi, le Shiphmite, était responsable de l'accroissement des vignes pour les caves à vin.
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
Baal Hanan, de Guéder, était responsable des oliviers et des sycomores qui se trouvaient dans la plaine. Joas était responsable des caves à huile.
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
Le chef des troupeaux qui paissaient dans le Saron était Shitrai, le Saronite. Le chef des troupeaux qui paissaient dans les vallées était Shaphat, fils d'Adlaï.
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
Responsable des chameaux: Obil, d'Ismaël. Jehdeiah, de Meronoth, était responsable des ânes. Sur les troupeaux, Jaziz, le Hagrite.
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
Tous ceux-là étaient les chefs de la propriété du roi David.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Jonathan, l'oncle de David, était aussi un conseiller, un homme intelligent et un scribe. Jehiel, fils de Hachmoni, était avec les fils du roi.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
Ahithophel était le conseiller du roi. Huschaï, l'Architecte, était l'ami du roi.
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
Après Achitophel, il y avait Jehojada, fils de Benaja, et Abiathar. Joab était le chef de l'armée du roi.

< 1 Nyakati 27 >