< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
Forsothe the sones of Israel bi her noumbre, the princes of meynees, the tribunes, and centuriouns, and prefectis, that mynystriden to the kyng bi her cumpenyes, entrynge and goynge out bi ech monethe in the yeer, weren souereyns, ech bi hym silf, on foure and twenti thousynde.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
Isiboam, the sone of Zabdihel, was souereyn of the firste cumpenye in the firste monethe, and vndur hym weren foure and twenti thousynde;
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
of the sones of Fares was the prince of alle princes in the oost, in the firste monethe.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Dudi Achoites hadde the cumpany of the secounde monethe, and aftir hym silf he hadde another man, Macelloth bi name, that gouernede a part of the oost of foure and twenti thousynde.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
And Bananye, the sone of Joiada, the preest, was duyk of the thridde cumpenye in the thridde monethe, and four and twenti thousynde in his departyng;
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
thilke is Bananye, the strongest among thritti, and aboue thritti; forsothe Amyzadath, his sone, was souereyn of his cumpenye.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the fourthe monethe, the fourthe prince was Asahel, the brother of Joab, and Zabadie, his sone, aftir hym, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the fifthe monethe, the fifthe prince was Samoth Jezarites, and foure and twenti thousynde in his cumpenye.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the sixte monethe, the sixte prince was Ira, the sone of Actes, Techuytes, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the seuenthe monethe, the seuenthe prince was Helles Phallonites, of the sones of Effraym, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the eiythe monethe, the eiythe prince was Sobothai Assothites, of the generacioun of Zarai, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the nynthe monethe, the nynthe prince was Abiezer Anathotites, of the generacioun of Gemyny, and foure and tweynti thousynde in his cumpeny.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the tenthe monethe, the tenthe prince was Maray, and he was Neophatites, of the generacioun of Zaray, and foure and twenti thousynde in his cumpany.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the elleuenthe monethe, the elleuenthe prince was Banaas Pharonytes, of the sones of Effraym, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
In the tweluethe monethe, the tweluethe prince was Holdia Nethophatites, of the generacioun of Gothonyel, and foure and twenti thousynde in his cumpeny.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
Forsothe these weren souereyns of the lynages of Israel; duyk Eliezer, sone of Zechri, was souereyn to Rubenytis; duyk Saphacie, sone of Maacha, was souereyn to Symeonytis;
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
Asabie, the sone of Chamuel, was souereyn to Leuytis; Sadoch `was souereyn to Aaronytis;
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
Elyu, the brothir of Dauid, `was souereyn to the lynage of Juda; Amry, the sone of Mychael, `was souereyn to Isacharitis;
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
Jesmaye, the sone of Abdie, was souereyn to Zabulonytis; Jerymuth, the sone of Oziel, `was souereyn to Neptalitis;
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
Ozee, the sone of Ozazym, `was souereyn to the sones of Effraym; Johel, the sone of Phatae, was souereyn to the half lynage of Manasses;
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
and Jaddo, the sone of Zacarie, `was souereyn to the half lynage of Manasses in Galaad; sotheli Jasihel, the sone of Abner, `was souereyn to Beniamyn; forsothe Ezriel,
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
the sone of Jeroam, was souereyn to Dan; these weren the princes of the sones of Israel.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
Forsothe Dauid nolde noumbre hem with ynne twenti yeer, for the Lord seide, that he wolde multiplie Israel as the sterris of heuene.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Joab, the sone of Saruye, bigan for to noumbre, and he fillide not; for ire fel on Israel for this thing, and therfor the noumbre of hem, that weren noumbrid, was not teld in to the bookis of cronyclis of kyng Dauid.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Forsothe Azymoth, the sone of Adihel, was on the tresouris of the kyng; but Jonathan, the sone of Ozie, was souereyn of these tresours, that weren in cytees, and in townes, and in touris.
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
Sotheli Ezri, the sone of Chelub, was souereyn on the werk of hosebondrie, and on erthe tiliers, that tiliden the lond;
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
and Semeye Ramathites was souereyn on tilieris of vyneris; sotheli Zabdie Aphonytes was souereyn on the wyn celeris;
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
for Balanam Gadaritis was on the olyue placis, and fige places, that weren in the feeldi places; sotheli Joas was on the schoppis, `ether celeris, of oile;
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
forsothe Cethray Saronytis `was souereyn of the droues, that weren lesewid in Sarena; and Saphat, the sone of Abdi, was ouer the oxis in valeys;
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
sotheli Vbil of Ismael was ouer the camelis; and Jadye Meronathites was ouer the assis; and Jazir Aggarene was ouer the scheep;
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
alle these weren princes of the catel of kyng Dauid.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Forsothe Jonathas, brother of `Dauithis fader, was a councelour, a myyti man, and prudent, and lettrid; he and Jahiel, the sone of Achamony, weren with the sones of the kyng.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
Also Achitofel was a counselour of the kyng; and Chusi Arachites was a frend of the kyng.
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
Aftir Achitofel was Joiada, the sone of Banaye, and Abyathar; but Joab was prince of the oost of the kyng.

< 1 Nyakati 27 >