< 1 Nyakati 26 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
Et quant aux départements des portiers; il y eut pour les Corites, Mésélémia fils de Coré, d'entre les enfants d'Asaph.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
Et les enfants de Mésélémia furent, Zacharie le premier-né; Jédihaël le second; Zébadia le troisième; Jathniël le quatrième,
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Hélam le cinquième, Johanum le sixième; Eliehohenaï le septième.
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
Et les enfants de Hobed-Edom furent, Sémahja le premier-né, Jéhozabad le second, Joah le troisième, Sacar le quatrième, Nathanaël le cinquième,
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
Hammiel le sixième, Issacar le septième, Pehulletaï le huitième; car Dieu l'avait béni.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
Et à Sémahja son fils naquirent des enfants, qui eurent le commandement sur la maison de leur père, parce qu'ils étaient hommes forts et vaillants.
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
Les enfants donc de Sémahja furent, Hothni, et Réphaël, Hobed, et Elzabad, ses frères, hommes vaillants, Elihu et Sémacia.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
Tous ceux-là étaient des enfants d'Hobed-Edom, eux et leurs fils, et leurs frères, hommes vaillants, et forts pour le service; ils étaient soixante-deux d'Hobed-Edom.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
Et les enfants de Mésélémia avec ses frères étaient dix-huit, vaillants hommes.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
Et les enfants de Hoza, d'entre les enfants de Mérari, furent Simri le Chef; car quoiqu'il ne fût pas l'aîné, néanmoins son père l'établit pour Chef.
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
Hilkija était le second, Tebalia le troisième, Zacharie le quatrième; tous les enfants et frères de Hoza furent treize.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
On fit à ceux-là les départements des portiers, en sorte que les charges furent distribuées aux Chefs de famille, en égalant les uns aux autres, afin qu'ils servissent dans la maison de l'Eternel.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
Car ils jetèrent les sorts autant pour le plus petit que pour le plus grand, selon leurs familles, pour chaque porte.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
Et ainsi le sort [pour la porte] vers l'Orient échut à Sélémia. Puis on jeta le sort pour Zacharie son fils, sage conseiller, et son sort échut [pour la porte] vers le Septentrion.
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
Le sort d'Hobed-Edom échut [pour la porte] vers le Midi, et la maison des assemblées échut à ses fils.
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
A Suppim et à Hosa [pour la porte] vers l'Occident, auprès de la porte de Salleketh, au chemin montant; une garde [étant] vis-à-vis de l'autre.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
Il y avait vers l'Orient, six Lévites; vers le Septentrion, quatre par jour; vers le Midi, quatre aussi par jour; et vers [la maison] des assemblées deux de chaque côté.
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
A Parbar vers l'Occident, il y en avait quatre au chemin, [et] deux à Parbar.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
Ce sont là les départements des portiers pour les enfants des Corites, et pour les enfants de Mérari.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
Ceux-ci aussi étaient Lévites; Ahija commis sur les trésors de la maison de Dieu, et sur les trésors des choses consacrées.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
Des enfants de Lahdan, qui étaient d'entre les enfants des Guersonites; du côté de Lahdan, d'entre les Chefs des pères appartenant à Lahdan Guersonite, Jéhiëli.
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
D'entre les enfants de Jéhiëli, Zétham, et Joël son frère, commis sur les trésors de la maison de l'Eternel.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
Pour les Hamramites, Jitsharites, Hébronites, et Hoziëlites.
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
Et Sébuël fils de Guersom, fils de Moïse, était commis sur les autres trésors.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
Et quant à ses frères du côté d'Elihézer, dont Réhabia fut fils, qui eut pour fils Esaïe, qui eut pour fils Joram, qui eut pour fils Zicri, qui eut pour fils Sélomith.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
Ce Sélomith et ses frères furent commis sur les trésors des choses saintes que le Roi David, les Chefs des pères, les Gouverneurs de milliers, et de centaines; et les Capitaines de l'armée avaient consacrées;
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
Qu'ils avaient, dis-je, consacrées des batailles et des dépouilles, pour le bâtiment de la maison de l'Eternel.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
Et tout ce qu'avait consacré Samuël le voyant, et Saül fils de Kis, et Abner fils de Ner, et Joab fils de Tséruïa; tout ce, enfin, qu'on consacrait, était mis entre les mains de Sélomith et de ses frères.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
D'entre les Jitsharites, Kénania et ses fils [étaient employés] aux affaires de dehors sur Israël, pour être prévôts et juges.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
Quant aux Hébronites, Hasabia et ses frères, hommes vaillants, au nombre de mille sept cents, [présidaient] sur le gouvernement d'Israël au deçà du Jourdain, vers l'Occident, pour tout ce qui concernait l'Eternel, et pour le service du Roi.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
Quant aux Hébronites, selon leurs générations dans les familles des pères, Jérija fut le Chef des Hébronites. On en fit la recherche en la quarantième année du règne de David, et on trouva parmi eux à Jahzer de Galaad des hommes forts et vaillants.
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
Les frères donc de [Jérija], hommes vaillants, furent deux mille sept cents, issus des Chefs des pères; et le Roi David les établit sur les Rubénites, sur les Gadites, et sur la demi-Tribu de Manassé, pour tout ce qui concernait Dieu, et pour les affaires du Roi.

< 1 Nyakati 26 >