< 1 Nyakati 26 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
Les classes des portiers. Des Corites: Meshélémia, fils de Koré, des fils d’Asaph.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
Et Meshélémia avait des fils: Zacharie, le premier-né; Jediaël, le second; Zebadia, le troisième; Jathniel, le quatrième;
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Élam, le cinquième; Jokhanan, le sixième; Élioénaï, le septième.
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
– Et les fils d’Obed-Édom: Shemahia, le premier-né; Jozabad, le second; Joakh, le troisième; et Sacar, le quatrième; et Nethaneël, le cinquième;
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
Ammiel, le sixième; Issacar, le septième; Peülthaï, le huitième, car Dieu l’avait béni.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
– Et à Shemahia, son fils, naquirent des fils qui gouvernèrent dans la maison de leur père, car ils étaient hommes forts et vaillants.
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
Les fils de Shemahia: Othni, et Rephaël, et Obed, Elzabad, [et] ses frères, hommes vaillants, Élihu et Semakia.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
Tous ceux-là étaient des fils d’Obed-Édom; eux, et leurs fils, et leurs frères, hommes vaillants et forts pour le service, 62, d’Obed-Édom.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
– Et Meshélémia avait des fils et des frères, hommes vaillants, 18.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
– Et Hosa, d’entre les fils de Merari, avait des fils: Shimri, le chef; bien qu’il ne soit pas le premier-né, son père l’établit pour chef;
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
Hilkija, le second; Tebalia, le troisième; Zacharie, le quatrième: tous les fils et les frères de Hosa étaient 13.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
À ceux-là furent les départements des portiers, aux chefs des hommes [qui vaquaient] à leurs charges avec leurs frères, pour faire le service dans la maison de l’Éternel.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
Et ils jetèrent les sorts, le petit comme le grand, selon leurs maisons de pères, pour chaque porte.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
Et le sort qui échut à Shélémia fut le levant; et on jeta le sort pour Zacharie, son fils, sage conseiller, et le sort qui lui échut fut le nord;
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
à Obed-Édom [échut] le midi; et à ses fils, la maison des approvisionnements;
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
à Shuppim et à Hosa, le couchant, avec la porte de Shalléketh, au chemin qui monte, une garde vis-à-vis de l’autre.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
Au levant, il y avait six Lévites; au nord, quatre par jour; au midi, quatre par jour; et aux approvisionnements, deux [et] deux;
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
à Parbar, vers le couchant, quatre au chemin, deux à Parbar.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
– Ce sont là les départements des portiers, d’entre les fils des Corites et d’entre les fils de Merari.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
Et les Lévites: Akhija était [préposé] sur les trésors de la maison de Dieu et sur les trésors des choses saintes.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
Les fils de Lahdan, les fils des Guershonites de Lahdan, les chefs des pères de Lahdan, le Guershonite: Jekhiéli;
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
les fils de Jekhiéli: Zétham et Joël, son frère, [préposés] sur les trésors de la maison de l’Éternel.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
Des Amramites, des Jitseharites, des Hébronites, des Uziélites…
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
Et Shebuel, fils de Guershom, fils de Moïse, était surintendant des trésors.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
Et ses frères, d’Éliézer: Rekhabia, son fils, et Ésaïe, son fils, et Joram, son fils, et Zicri, son fils, et Shelomith, son fils.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
Ce Shelomith et ses frères furent [préposés] sur tous les trésors des choses saintes que le roi David, et les chefs des pères, les chefs de milliers et de centaines, et les chefs de l’armée, avaient consacrées,
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
qu’ils avaient consacrées, des guerres et du butin, pour l’entretien de la maison de l’Éternel;
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
et tout ce qu’avaient consacré Samuel, le voyant, et Saül, fils de Kis, et Abner, fils de Ner, et Joab, fils de Tseruïa: tout ce qui était consacré était [mis] sous la main de Shelomith et de ses frères.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
D’entre les Jitseharites, Kenania et ses fils étaient [établis] sur Israël pour les affaires extérieures, comme intendants et juges.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
D’entre les Hébronites, Hashabia et ses frères, hommes vaillants, [au nombre de] 1 700, pour l’administration d’Israël, en deçà du Jourdain, vers le couchant, pour toutes les affaires de l’Éternel et pour le service du roi.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
D’entre les Hébronites, Jerija fut le chef; (on rechercha les Hébronites, selon leurs générations, selon les pères, en la quarantième année du règne de David, et on trouva parmi eux, à Jahzer de Galaad, des hommes forts et vaillants; )
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
et ses frères, hommes vaillants, étaient 2 700, des chefs des pères; et le roi David les établit sur les Rubénites et sur les Gadites et sur la demi-tribu des Manassites, pour toutes les affaires de Dieu et pour les affaires du roi.

< 1 Nyakati 26 >