< 1 Nyakati 26 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
This is a list of the groups of men who guarded the temple gates: From the descendants of Korah, there was Meshelemiah, the son of Kore, who was one of the sons of Asaph.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
The oldest son of Meshelemiah was Zechariah. His other sons were Jediael, Zebadiah, Jathniel,
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Elam, Jehohanan, and Eliehoenai.
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
[Another guard] was Obed-Edom. His oldest son was Shemaiah. His other sons were Jehozabad, Joah, Sacar, Nethanel,
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
Ammiel, Issachar, and Peullethai. It was because God had blessed him that he had many sons.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
Obed-Edom’s son Shemaiah also had sons. They were leaders in their father’s family because they were capable of doing many things well.
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
The sons of Shemaiah were Othni, Rephael, Obed, and Elzabad. Shemaiah’s relatives Elihu and Semakiah were also capable men.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
All of those descendants of Obed-Edom and their sons and relatives were capable people and strong workers. Altogether there were 62 of them.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
Another guard was Meshelemiah. He and his sons and relatives were also capable people. There were 18 of them altogether.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
Another guard was Hosah’s son Shimri, a descendant of Merari. Hosah appointed Shimri to be the leader, even though he was not Hosah’s oldest son.
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
Hosah’s other sons were Hilkiah, Tabaliah, and Zechariah. Altogether there were 13 sons and relatives of Hosah.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
Those men were leaders of the groups of men who guarded the gates of the temple. They worked at the temple like their relatives did.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
By casting lots, the leader of each family chose one gate for their group to guard. [All of them, including] young men and old men (OR, including leaders of large families and small families), cast lots.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
Shelemiah’s group was selected to guard the East Gate. The group of Shelemiah’s son Zechariah, who was a wise counselor, was selected to guard the North Gate.
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
Then Obed-Edom’s group was selected to guard the South Gate, and his sons were selected to guard the [entrances to the temple] storerooms.
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
Then Shuppim’s group and Hosah’s group were selected to guard the West Gate and the Shalleketh Gate on the upper road [to the temple]. The work for the guards was divided evenly.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
Each day there were six descendants of Levi who guarded the East Gate, four who guarded the North Gate, four who guarded the South Gate, and two at a time who guarded the entrances to the storerooms.
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
At the West gate there were two men who guarded the courtyard and four who guarded the road outside the courtyard.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
Those were the groups of men who were descendants of Korah and Merari who guarded the gates [of the temple].
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
Other descendants of Levi were in charge of the chests that contained the money that was dedicated to Yahweh, money that the people brought to the temple.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
[One of those men was] Ladan, a descendant of Gershon. He was the ancestor of several family groups. Jehiel was the leader of one of those family groups.
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
Others who had that work were Zetham and his [younger] brother Joel, who were the sons of Jehiel.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
Others who did that work were descendants of Amram, Izhar, Hebron and Uzziel.
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
[From the descendants of Amram], Shubael, a descendant of Moses’s son Gershom, was the leader who was in charge of the money chests.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
[Others who did that work were] the descendants of [Gershom’s younger brother] Eliezer. Those men were Eliezer’s son Rehabiah, Rehabiah’s son Jeshaiah, Jeshaiah’s son Joram, Joram’s son Zicri, and Zicri’s son Shelomith.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
Shelomith and his relatives were in charge of all the valuable things that had been dedicated [to Yahweh] by King David, by the leaders of the family groups, by the army commanders of 1,000 soldiers and commanders of 100 soldiers, and by other army commanders.
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
Some of the things that those army officers had taken [from Israel’s enemies] in battles they dedicated for the repair of the temple of Yahweh.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
And Shelomith and his relatives were also in charge of everything that had been dedicated [to Yahweh] by the prophet Samuel, by King Saul, and by [David’s two army commanders] Ner and Joab.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
From the descendants of Izhar, Kenaniah and his sons were given work outside [the temple area]. They were officials and judges in [various places] in Israel.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
From the descendants of Hebron, Hashabiah and his relatives were responsible for the work done for Yahweh and for the king in all the area west of the Jordan [river]. There were 1,700 of them who were able to do their work well.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
It was written in the records of the descendants of Hebron that Jeriah was their leader. When David had been ruling for almost 40 years, they searched in those records, and they found [names of] capable men descended from Hebron who were at Jazer [city] in the Gilead [region].
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
Jeriah had 2,700 relatives who were able to do their work well, and who were leaders of their families. King David put them in charge of governing the tribes of Reuben, Gad, and [the eastern] half of the tribe of Manasseh, to be sure that all the people did what God and the king told them to do.

< 1 Nyakati 26 >