< 1 Nyakati 26 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
Concerning the divisions of the gatekeepers [who were] of the Korchites: Meshelemyahu the son of Kore, of the sons of Assaph.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
And Meshelemyahu had sons: Zecharyahu the first-born, Jedi'ael the second, Zebaiyahu the third, Jathniel the fourth,
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Elam the fifth, Jehochanan the sixth, Elyeho'enal the seventh,
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
And 'Obed-edom had sons: Shema'yah the first-born, Jehosabad the second, Joach the third, and Sachar the fourth, and Nethanel the fifth,
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
'Ammiel the sixth, Issachar the seventh, Pe'ulthai the eighth; for God had blessed him.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
Also unto Shema'yah his son there were born sons, that were rulers for the house of their father; for they were mighty men of valor.
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
The sons of Shema'yah were 'Othni, and Rephael, and 'Obed, [and] Elsahad, his brothers [were] valiant men, Elihu, and Semachyahu.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
All these were of the sons of 'Obed-edom: they and their sons and their brethren were valiant men in strength for the service, being sixty and two [descendants] of 'Obed-edom.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
And Meshelemyahu had sons and brethren, valiant men, eighteen.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
Also Chossah, of the children of Merari, had sons: Shimri the chief, for [though] he was not the first-born, yet his father made him the chief;
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
Chilkiyahu the second, Tehalyahu the third, Zecharyahu the fourth; all the sons and brethren of Chossah were thirteen.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
These divisions of the gatekeepers, after the chief men, had the watch along with their brethren, to minister in the house of the Lord.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
And they cast lots, the small as well as the great, according to their family divisions, for each and every gate.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
And the lot at the east fell for Shelemyahu. And for Zecharyahu his son, an intelligent counsellor, they cast lots, and his lot came out at the north.
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
For 'Obed-edom at the south; and to his sons [was assigned] the house of Assuppim.
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
For Shuppim and for Chossah at the west, by the gate Shallecheth, on the ascending causeway, watch alongside of watch.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
At the east were six Levites, at the north four for every day, at the south four for every day, and for [the house of] Assuppim always two.
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
At the Parbar on the west, four at the causeway, and two at the Parbar.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
These are the divisions of the gatekeepers of the sons of the Korchites, and of the sons of Merari.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
And of the Levites, Achiyah was over the treasuries of the house of God, and over the treasuries of the holy things.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
[As concerning] the sons of La'dan, the sons of the Gershunites of La'dan, the chiefs of the families of La'dan the Gershunite, were the Jechielites.
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
The sons of Jechieli, Zetham, and Joel his brother, were over the treasuries of the house of the Lord.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
Of the 'Amramites, of the Yizharites, of the Hebronites, and of the 'Uzzielites,
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
[Was] even Shebuel the son of Gershom, the son of Moses, superintendent of the treasuries.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
And his brethren by Eli'ezer: Rechabyahu his son, and Jesha'yahu his son, and Joram his son, and Zichri his son, and Shelomoth his son.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
This Shelomoth and his brethren were over all the treasuries of the holy things, which king David had sanctified, together with the chiefs of the family divisions, the captains over the thousands and the hundreds, and the captains of the army.
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
Out of the wars, and out of the booty did they sanctify to maintain the house of the Lord.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
And all that Samuel the seer, and Saul the son of Kish, and Abner the son of Ner, and Joab the son of Zeruyah, had sanctified, whatsoever [any one] had sanctified, was under the supervision of Shelomoth and of his brethren.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
Of the Yizharites were Kenanyahu and his sons for the outward business over Israel, for officers and judges.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
Of the Hebronites were Chashabyahu and his brethren, valiant men, a thousand and seven hundred [in number], appointed over the affairs of Israel on this side of the Jordan to the west, for all the business of the Lord, and for the service of the king.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
Of the Hebronites was Jeriyah the chief, for the Hebronites, according to their generations by families. In the fortieth year of the reign of David were they inquired into, and there were found among them mighty men of valor at Ja'zer of Gil'ad.
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
And his brethren, valiant men, were two thousand and seven hundred chiefs of families: and king David appointed them over the Reubenites, the Gadites, and the half tribe of Menasseh, for every matter pertaining to God, and the affairs of the king.

< 1 Nyakati 26 >