< 1 Nyakati 26 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
This is a list of the divisions of the gatekeepers. From the Korahites: Meshelemiah son of Kore, one of the sons of Asaph.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
The sons of Meshelemiah: Zechariah (first), Jediael (second), Zebadiah (third), Jathniel (fourth),
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Elam (fifth), Jehohanan (sixth), and Eliehoenai (seventh).
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
The sons of Obed-edom: Shemaiah (first), Jehozabad (second), Joah (third), Sacar (fourth), Nethanel (fifth),
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
Ammiel (sixth), Issachar (seventh), and Peullethai (eighth), for God had blessed Obed-edom.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
Shemaiah, Obed-edom's son, had sons who were capable leaders and had great authority in their father's family
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
The sons of Shemaiah: Othni, Rephael, Obed, and Elzabad. His relatives, Elihu and Semakiah, were also capable men.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
All these descendants of Obed-edom, plus their sons and grandsons, a total of sixty-two, were capable men, well qualified for their service.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
Meshelemiah's eighteen sons and brothers were also capable men.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
Hosah, one of the sons of Merari, made Shimri as leader among his sons, though he was not the firstborn.
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
His other sons included Hilkiah (second), Tebaliah (third), and Zechariah (fourth). The total of Hosah's sons and relatives was thirteen.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
These divisions of the gatekeepers, through their family leaders, served in the house of the Lord, just like their brothers.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
Every gate was assigned by lot to different families, the least important equal to the most important.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
The lot for the east gate fell to Meshelemiah. Then they cast lots for his son Zechariah, a wise counselor with insight, and the lot for the north gate fell to him.
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
The lot for the south gate fell to Obed-edom, and the lot for the storehouse fell to his sons.
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
Shuppim and Hosah received the west gate and the gate of Shallecheth on the road that leads up. They were always guarded.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
There were six Levites on duty every day at the east gate, four at the north gate, four at the south gate, and two at a time at the storehouse.
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
Six were on duty every day at the west gate, four at the main road, and two at the courtyard.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
These were the divisions of the gatekeepers from the sons of Korah and the sons of Merari.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
Other Levites under Ahijah were in charge of the treasuries of the house of God and the treasuries of the what had been dedicated to God.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
From the sons of Ladan, who were the descendants of the Gershonites through Ladan, and were the family leaders of Ladan the Gershonite: Jehieli.
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
The sons of Jehieli, Zetham and his brother Joel, were in charge of the treasuries of the house of the Lord.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
From the Amramites, the Izharites, the Hebronites, and the Uzzielites:
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
Shebuel, a descendant of Gershom, son of Moses, who was the chief officer in charge of the treasuries.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
His relatives by Eliezer were Rehabiah, Jeshaiah, Joram, Zicri, and Shelomoth.
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
Shelomoth and his relatives were in charge of all the treasuries for all that had been dedicated by King David, by the family leaders who were the commanders of thousands and of hundreds, and by the army commanders.
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
They dedicated a part of the plunder they had won in battle to help maintain the house of the Lord.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
Shelomoth and his relatives also looked after the gifts dedicated to the Lord by Samuel the seer, Saul son of Kish, Abner son of Ner, and Joab son of Zeruiah. All the dedicated gifts were the responsibility of Shelomoth and his relatives.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
From the Izharites: Kenaniah and his sons were given outside duties as officials and judges over Israel.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
From the Hebronites: Hashabiah and his relatives, 1,700 capable men, were put in charge of the Israel west of the Jordan, responsible for everything involving the Lord's work and the king's service.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
Also from the Hebronites came Jerijah, the leader of the Hebronites according to the family genealogies. In the fortieth year of David's reign the records were examined, and men of great ability were discovered at Jazer in Gilead.
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
Among the relatives of Jerijah were 2,700 capable men who were family leaders. King David put them in charge of the tribes of Reuben and Gad and the half-tribe of Manasseh. They were responsible for everything involving the Lord's work and the king's service.