< 1 Nyakati 26 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
За отредите на вратарите: от Кореевите бе Меселемия, Кореевият потомец, от Асафовите синове.
2 Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
А Меселемиеви синове бяха: Захария, първородният; Едиил, вторият; Зевадия, третият; Ятниил, четвъртият;
3 Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
Елам, петият; Иоанан, шестият; и Елиоинай, седмият.
4 Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
И Овид-едомови синове: Семаия, първородният; Иозавад, вторият; Иоах третият; Сахар четвъртият; Натанаил, петият;
5 Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
Амиил, шестият; Исахар, седмият; и Феулатай, осмият; защото Бог го благослови.
6 Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
А на сина му Семаия се родиха синове, които властвуваха над бащиния си дом, защото бяха силни и храбри мъже:
7 Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
Семаевите синове бяха: Офний Рафаил, Овид, Елзавад, чиито братя, Елиу и Семахия, бяха шестдесет и двама души.
8 Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
Всички тия от Овид-едомовите потомци, те, синовете им и братята им от Овид-едома, силни и способни за службата, бяха шестдесет и двама души.
9 Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
А Меселемия имаше осемнадесет храбри синове и братя.
10 Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
А синовете на Оса от Мерариевите потомци бяха: Симрий, първият, (защото, ако и да не беше първороден, пак баща му го направи пръв);
11 Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
Хелкия, вторият; Тевалия, третият: и Захария четвъртият, Всичките синове и братя на Оса бяха тринадесет души.
12 Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
От тия се образуваха отредите на вратарите, ще каже на главните мъже, имащи заръчвания наравно с братята си да слугуват в Господния дом.
13 Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
И за всяка порта хвърлиха жребий, малък и голям еднакво според бещините си домове.
14 Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
И жребият за Селемия падна към изток. Тогава хвърлиха жребий за сина му Захария, мъдър съветник; и на него жребият излезе към север;
15 Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
за Овид-едома към юг, а за синовете му влагалището;
16 Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
за Суфима и Оса към запад, с портата Салехет, при пътя, който върви нагоре, стража слещу стража.
17 Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
Към изток бяха шестима левити, към север четирима на ден, към юг четирима на ден, и към влагалището по двама;
18 Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
в Първото към запад, четирима към пътя, който върви на горе, и двама в Парвар.
19 Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
Тия бяха отредите на вратарите между кореевите потомци и Мерариевите потомци.
20 Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
А от левитите Ахия бе над съкровищата на Божия дом и над съкровищата на посветените неща.
21 Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
Ладанови синове: синовете на гирсонеца Ладан, началници на бащини домове на гирсонеца Ладан, бяха Ехиил;
22 wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
а Ехииловите синове, Зетан и брат му Иоил, бяха над съкровищата на Господния дом.
23 Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
От Амрамовците, Исааровците, Хевроновците и Озииловците,
24 Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
Суваил, син на Гирсама, Моисеевия син, бе надзирател над съкровищата.
25 Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
А братята му от Елиезера, чийто син бе Равия, а негов син Исаия, негов син Иорам, негов син Зехрий, а негов син Селомит;
26 Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
тоя Селомит и братята му бяха над всичките съкровища на посветените неща, които посветиха цар Давид, първенците на бащините домове, хилядниците, стотниците и военачалниците.
27 Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
От користите, вземани в боевете, бяха посветили за построяването на Господния дом.
28 Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
Също и всичко, каквото бяха посветили гледачът Самуил, Саул Кисовият син, Авенир Нировият син, и Иоав Саруиният син, - всичко посветено от кого да било, - бе под ръката на Селомита и на братята му.
29 Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
От Исааровците: Ханания и синовете му бяха надзиратели и съдии над Израиля за външните дела.
30 Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
От Хевроновците: Асавия и братята му, хиляда и седемстотин храбри мъже, бяха надзиратели над Израиля отсам Иордан, на запад, за всичките Господни дела и за слугуването на царя.
31 Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
Между Хевроновците Ерия беше началник, между Хевроновците, според поколенията им, според бащините им домове. В четиридесетата година на Давидовото царуване те бяха прегледани, и между тях се намериха силни и храбри мъже в Язир Галаад.
32 Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.
И братята му, храбри мъже, бяха две хиляди и седемстотин началници на бащини домове, които цар Давид постави над Рувимците, гадците и половината Манасиево племе за всяко божие дело и за царските работи.

< 1 Nyakati 26 >