< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Ahora, las divisiones en que se agruparon los hijos de Aarón fueron estas: los hijos de Aarón, Nadab y Abiú, Eleazar e Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Pero Nadab y Abiú llegaron a su fin antes que su padre, y no tuvieron hijos; así hicieron Eleazar e Itamar el trabajo de los sacerdotes.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
Y David, con Sadoc de los hijos de Eleazar y Ahimelec de los hijos de Itamar, los repartió en sus puestos para su trabajo.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Y hubo más jefes entre los hijos de Eleazar que entre los hijos de Itamar; y así se agruparon: de los hijos de Eleazar había dieciséis, todos jefes de familia; y de los hijos de Itamar, jefes de familia, había ocho.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Así que fueron agrupados, por decisión del Señor, uno con el otro; porque había gobernantes del lugar santo y gobernantes de la casa de Dios entre los hijos de Eleazar y los hijos de Itamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Entonces Semaías, hijo de Nethanel, escriba, que era levita, escribió sus nombres por escrito: el rey estaba presente con los gobernantes, y el sacerdote Sadoc, y Ahimelec, hijo de Abiatar, y jefes de familia de los sacerdotes y los levitas; una familia tomada para Eleazar y luego una para Ithamar, y así sucesivamente.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Y el primer nombre que salió fue el de Joiarib; el segundo jedaias;
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
El tercer Harim; el cuarto Seorim;
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
El quinto Malquias; el sexto Mijamin;
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
El séptimo Cos; el octavo Abías;
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
El noveno Jesúa; el décimo Secanías;
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
El undécimo Eliasib; el duodécimo Jaquim;
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
La decimotercera Hupa; el decimocuarto jesebeab;
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
La quinceava Bilga; la decimosexta Imer;
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
El decimoséptimo Hezir; el decimoctavo Afses;
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
El decimonoveno de Petaias; el vigésimo Hezequiel;
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
El vigésimo primero Jaquin; el vigésimo segundo Gamul;
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
El vigésimo tercer Delaía; el vigésimo cuarto Maazías.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Así que fueron puestos en sus diferentes grupos, para tomar sus lugares en la casa del Señor, de acuerdo con las reglas establecidas por su padre Aarón, como el Señor, el Dios de Israel, le había dado órdenes.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Y del resto de los hijos de Leví: de los hijos de Amram, Subael; de los hijos de Subael, Jehdeías.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
De los hijos de Rehabiah, Isias él mayor.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
De los Izhar, Selomot; de los hijos de Selomot, Jahat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
Y los hijos de Hebrón: Jerías el primero; Amarías, el segundo; Jahaziel el tercero; Jacaman, el cuarto.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Los hijos de Uziel, Micaia; de los hijos de Miqueas, Samir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
El hermano de Miqueas, Isias; de los hijos de Isias, Zacarías.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
Los hijos de Merari: Mahli y Musi; Los hijos de Jaazías.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
Los hijos de Merari: de Jaazias, Soham y Zacur e Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
De Mahli: Eleazar, que no tuvo hijos.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
De Cis: los hijos de Kish, Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
Y los hijos de Musi: Mahli, Edar y Jerimot. Estos fueron los hijos de los levitas por sus familias.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
La selección se hizo de estos de la misma manera que de sus hermanos, los hijos de Aarón, estando presente David el rey, con Sadoc, y Ahimelec, y los jefes de familia de los sacerdotes y de los levitas.

< 1 Nyakati 24 >