< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
अहरोन-वंशजों के समूह ये थे: अहरोन के पुत्र थे नादाब, अबीहू, एलिएज़र और इथामार.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
मगर नादाब और अबीहू की मृत्यु उनके पिता के देखते-देखते हो गई थी. उनके कोई संतान भी न थी. फलस्वरूप एलिएज़र और इथामार ने पौरोहितिक कार्यभार अपने ऊपर ले लिया.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
एलिएज़र वंशज सादोक और इथामार-वंशज अहीमेलेख के साथ मिलकर दावीद ने सेवा के लिए उनके पदों के अनुसार उनके समूहों को बांट दिया.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
इसलिये कि एलिएज़र-वंशजों में इथामार-वंशजों से संख्या में ज्यादा मुख्य पाए गए, उनका बंटवारा इस प्रकार किया गया: एलिएज़र-वंशजों में सोलह और इथामार-वंशजों में आठ मुख्य पाए गए, ये दोनों ही उनके घरानों के अनुसार थे.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
पासा फेंकने की प्रथा के द्वारा इन सभी का बंटवारा किया गया था; बिना किसी भेद-भाव के सभी का, क्योंकि वे मंदिर के, हां, परमेश्वर के लिए चुने गए अधिकारी थे. ये दोनों ही एलिएज़र और इथामार-वंशज थे.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
लेवियों में से नेथानेल के पुत्र शेमायाह ने राजा, शासकों, पुरोहित सादोक, अबीयाथर के पुत्र अहीमेलेख और पुरोहितों के घरानों और लेवियों के सामने इन्हें लिख लिया. एक घराना एलिएज़र के लिए और एक घराना इथामार के लिए लिखा गया.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
इस प्रक्रिया से पहला पासा यहोइयारिब के लिए, दूसरा येदाइयाह के लिए,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
तीसरा हारिम के लिए, चौथा सेओरिम के लिए,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
पांचवां मालाखियाह के लिए, छठा मियामिन के लिए,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
सातवां हक्कोज़ के लिए, आठवां अबीयाह के लिए,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
नवां येशुआ के लिए, दसवां शेकानियाह के लिए,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
ग्यारहवां एलियाशिब के लिए, बारहवां याकिम के लिए,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
तेरहवां हुप्पाह के लिए, चौदहवां येशेबियाब के लिए,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
पन्द्रहवां बिलगाह के लिए, सोलहवां इम्मर के लिए,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
सत्रहवां हेज़ीर के लिए, अठारहवां हापीज़ीज़ के लिए,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
उन्नीसवां पेथाइयाह के लिए, बीसवां यहेजकेल के लिए,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
इक्कीसवां याकिन के लिए, बाईसवां गामुल के लिए,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
तेईसवां देलाइयाह के लिए और चौबीसवां माजियाह के लिए निकला.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
जब ये अपने पूर्वज अहरोन द्वारा दिए गए आदेश के अनुसार याहवेह के भवन में आए, उन्हें सेवा के लिए ये ही पद सौंपे गए थे-ठीक जैसा आदेश उन्हें याहवेह, इस्राएल के परमेश्वर ने दिया था.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
इनके अलावा लेवी के अन्य वंशजों का लेखा इस प्रकार है: अमराम के पुत्रों में से शेबुएल; शेबुएल के पुत्रों में से येहदेइया.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
रेहाबिया के पुत्रों में से इश्शियाह, जो जेठा भी था.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
इज़हारियों के वंशजों में से शेलोमोथ; शेलोमोथ के वंशजों में से याहाथ.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
हेब्रोन के पुत्र थे येरिया: जो जेठा भी था, अमरियाह छोटा था, याहाज़िएल तीसरा और येकामियम चौथा.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
उज्ज़िएल के पुत्रों में से मीकाह; मीकाह के पुत्रों में से शामीर.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
मीकाह का भाई था इश्शियाह; इश्शियाह के पुत्रों में से ज़करयाह.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
मेरारी के पुत्र माहली और मूशी; यआत्सियाह का पुत्र बेनो,
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
मेरारी के पुत्र: बेनो, शोहाम, ज़क्कूर और इबरी, जो यआत्सियाह से थे.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
माहली से एलिएज़र, जिसके कोई संतान न हुई.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
कीश से कीश के पुत्र थे: येराहमील.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
मूशी के पुत्र माहली एदर और येरीमोथ. ये सभी लेवियों के वंशज थे, जैसा उनके घराने द्वारा स्पष्ट है.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
ठीक अपने संबंधियों, अहरोन-वंशजों के समान, उन्होंने भी राजा दावीद, सादोक, अहीमेलेख, लेवियों और पुरोहितों के घरानों के प्रधानों के सामने अपने पासे फेंके. ये सभी घरानों के प्रधान भी थे और उनके छोटे भाइयों के कुल के भी.