< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Nämä olivat Aaronin poikien osastot: Aaronin pojat olivat Naadab, Abihu, Eleasar ja Iitamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Mutta Naadab ja Abihu kuolivat ennen isäänsä, eikä heillä ollut poikia. Niin palvelivat ainoastaan Eleasar ja Iitamar pappeina.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
Ja Daavid yhdessä Saadokin kanssa, joka oli Eleasarin poikia, ja Ahimelekin kanssa, joka oli Iitamarin poikia, jakoi heidät osastoihin heidän palvelusvuorojensa mukaan.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Kun Eleasarin pojilla havaittiin olevan enemmän päämiehiä kuin Iitamarin pojilla, jaettiin heidät niin, että Eleasarin pojat saivat kuusitoista päämiestä perhekunnilleen ja Iitamarin pojat kahdeksan päämiestä perhekunnilleen.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Heidät jaettiin arvalla, toiset niinkuin toisetkin, sillä pyhäkköruhtinaat ja Jumalan ruhtinaat otettiin sekä Eleasarin pojista että Iitamarin pojista.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Ja Semaja, Netanelin poika, kirjuri, joka oli Leevin sukua, kirjoitti heidät muistiin kuninkaan, päämiesten, pappi Saadokin ja Ahimelekin, Ebjatarin pojan, sekä pappien ja leeviläisten perhekuntien päämiesten läsnäollessa. Yksi perhekunta otettiin vuorotellen Eleasarin ja Iitamarin suvusta.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Ensimmäinen arpa tuli Joojaribille, toinen Jedajalle,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
kolmas Haarimille, neljäs Seoromille,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
viides Malkialle, kuudes Miijaminille,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
seitsemäs Koosille, kahdeksas Abialle,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
yhdeksäs Jeesualle, kymmenes Sekanjalle,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
yhdestoista Eljasibille, kahdestoista Jaakimille,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
kolmastoista Huppalle, neljästoista Jesebabille,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
viidestoista Bilgalle, kuudestoista Immerille,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
seitsemästoista Heesirille, kahdeksastoista Pissekselle,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
yhdeksästoista Petahjalle, kahdeskymmenes Hesekielille,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
kahdeskymmenes yhdes Jaakinille, kahdeskymmenes kahdes Gaamulille,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
kahdeskymmenes kolmas Delajalle, kahdeskymmenes neljäs Maasjalle.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Nämä ovat heidän palvelusvuoronsa, kun he menevät Herran temppeliin, niinkuin heidän isänsä Aaron oli heille säätänyt, sen mukaan, kuin Herra, Israelin Jumala, oli häntä käskenyt.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Mitä tulee muihin Leevin jälkeläisiin, niin oli Amramin jälkeläisiä Suubael, Suubaelin jälkeläisiä Jehdeja,
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Rehabjan jälkeläisiä päämies Jissia,
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
jisharilaisia Selomot, Selomotin jälkeläisiä Jahat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
Ja Jerian jälkeläisiä olivat: Amarja toinen, Jahasiel kolmas, Jekamam neljäs.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Ussielin jälkeläisiä oli Miika, Miikan jälkeläisiä Saamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
Miikan veli oli Jissia; Jissian jälkeläisiä oli Sakarja.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
Merarin jälkeläisiä olivat Mahli ja Muusi sekä hänen poikansa Jaasian jälkeläiset.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
Merarilla oli jälkeläisiä pojastaan Jaasiasta ynnä Sooham, Sakkur ja Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Mahlista polveutui Eleasar, jolla ei ollut poikia.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Kiisistä polveutui Jerahmeel, joka oli Kiisin jälkeläisiä.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
Ja Muusin jälkeläisiä olivat Mahli, Eeder ja Jerimot. Nämä olivat leeviläisten jälkeläiset heidän perhekuntiensa mukaan.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
Myöskin nämä, niinhyvin perhekuntapäämiehet kuin heidän nuoremmat veljensä, heittivät arpaa samoin kuin heidän veljensä, Aaronin pojat, kuningas Daavidin, Saadokin ja Ahimelekin sekä pappien ja leeviläisten perhekuntien päämiesten läsnäollessa.