< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Mutta tämä oli Aaronin lasten järjestys: Aaronin pojat oli: Nadab, Abihu, Eleasar ja Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Mutta Nadab ja Abihu kuolivat isänsä edessä, ja ei heillä ollut lasta. Ja Eleasar ja Itamar tulivat papeiksi.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
Ja David määräsi heitä näin: Zadokin Eleasarin lapsista ja Ahimelekin Itamarin lapsista, heidän virkansa jälkeen heidän palveluksessansa.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Ja usiammat väkevät päämiehet löydettiin Eleasarin kuin Itamarin lapsista, koska he heitä niin määräsivät: Eleasarin lapsista oli siellä kuusitoistakymmentä ylimmäistä heidän isäinsä huoneessa, ja kahdeksan Itamarin lapsista, heidän isäinsä huoneessa.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Ja he määräsivät heitä arvalla sekä näitä että niitä; sillä molemmat Eleasarin ja Itamarin lapset olivat päämiehet pyhässä ja päämiehet Jumalan edessä.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Ja Semaja kirjoittaja, Netaneelin poika Leviläisistä, kirjoitti heidät kuninkaan edessä, ja päämiesten ja papin Zadokin, ja Ahimelekin Abjatarin pojan, ja pappein ja Leviläisten, ja ylimmäisten isäin edessä: yksi isän huone otettiin Eleasarin edestä ja toinen otettiin sitte Itamarin edestä.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Ja ensimäinen arpa lankesi Jojaribin päälle, toinen Jedatjan,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
Kolmas Harimin, neljäs Seorimin,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
Viides Malkian, kuudes Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
Seitsemäs Hakkotsin, kahdeksas Abian,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
Yhdeksäs Jesuan, kymmenes Sekanian,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
Yksitoistakymmenes Eliasibin, kaksitoistakymmenes Jakimin,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
Kolmastoistakymmenes Huppan, neljästoistakymmenes Jesebabin,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
Viidestoistakymmenes Bilgan, kuudestoistakymmenes Immerin,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
Seitsemästoistakymmenes Hesirin, kahdeksastoistakymmenes Happitsetsin,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
Yhdeksästoistakymmenes Petahian, kahdeskymmenes Jeheskelin,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
Ensimäinenkolmattakymmentä Jakinin, toinenkolmattakymmentä Gamulin,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
Kolmaskolmattakymmentä Delajan, neljäskolmattakymmentä Maasian.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Tämä on heidän järjestyksensä heidän virkansa jälkeen, menemään Herran huoneesen tapansa jälkeen, isänsä Aaronin käden alla; niinkuin Herra Israelin Jumala heidän oli käskenyt.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Muiden Levin lasten seassa oli Amramin lapsista Subael, Subaelin lapsista Jehdeja.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Rehabian lapsista: Jissia oli heistä ensimäinen.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Mutta Jitseharilaisista oli Selomot, Selomotin lapsista Jahat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
(Hebronin lapset) Jerija ensimäinen, Amaria toinen, Jahasiel kolmas, Jekameam neljäs.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Ussielin lapset: Miika. Miikan lapsista Samir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
Jesija oli Miikan veli; Jesijan lapsista Sakaria.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
Merarin lapset: Maheli ja Musi; Jaesijan hänen poikansa lapset.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
Merarin lapset Jaesijasta, hänen poikansa oli Soham, Sakkur ja Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Mutta Mahelilla oli Eleasar, ja hänellä ei ollut yhtään poikaa.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Kisistä, Kisin lapset: Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
Musin lapset: Maheli, Eder ja Jeremot. Ne ovat Leviläisten lapset heidän isäinsä huoneen jälkeen.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
Ja nämät myös heittivät arpaa veljeinsä Aaronin lasten kanssa kuningas Davidin edessä, ja Zadokin ja Ahimelekin, ja ylimmäisten isäin edessä, pappein ja Leviläisten seassa; ylimmäinen isäin seassa pienimmänkin veljensä kanssa.