< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
La ordo de la Aaronidoj: la filoj de Aaron: Nadab, Abihu, Eleazar, kaj Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Nadab kaj Abihu mortis pli frue ol ilia patro, kaj filojn ili ne havis; kaj Eleazar kaj Itamar fariĝis pastroj.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
La ordon aranĝis David, kaj Cadok el la idoj de Eleazar, kaj Aĥimeleĥ el la idoj de Itamar, laŭ iliaj oficoj ĉe ilia servado.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Montriĝis, ke inter la idoj de Eleazar estis pli granda nombro da viroj, ol inter la idoj de Itamar. Oni dividis ilin: por la idoj de Eleazar estis dek ses ĉefoj de patrodomoj, kaj por la idoj de Itamar ok patrodomoj.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Oni dividis ilin per lotado, ambaŭ partojn paralele, ĉar la estroj de la sanktejo kaj la estroj en la aferoj de Dio estis el la idoj de Eleazar kaj el la idoj de Itamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Kaj enskribis ilin Ŝemaja, filo de Netanel, skribisto el la Levidoj, antaŭ la reĝo kaj la estroj, antaŭ la pastro Cadok, antaŭ Aĥimeleĥ, filo de Ebjatar, kaj antaŭ la ĉefoj de patrodomoj de la pastroj kaj de la Levidoj; unu loto estis por patrodomo de Eleazaridoj, kaj unu loto estis por patrodomo de Itamaridoj.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
La unua loto eliris por Jehojarib, la dua por Jedaja,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
la tria por Ĥarim, la kvara por Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
la kvina por Malkija, la sesa por Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
la sepa por Hakoc, la oka por Abija,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
la naŭa por Jeŝua, la deka por Ŝeĥanja,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
la dek-unua por Eljaŝib, la dek-dua por Jakim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
la dek-tria por Ĥupa, la dek-kvara por Jeŝebab,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
la dek-kvina por Bilga, la dek-sesa por Imer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
la dek-sepa por Ĥezir, la dek-oka por Hapicec,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
la dek-naŭa por Petaĥja, la dudeka por Jeĥezkel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
la dudek-unua por Jaĥin, la dudek-dua por Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
la dudek-tria por Delaja, la dudek-kvara por Maazja.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Tio estis ilia ordo ĉe ilia servado, por iri en la domon de la Eternulo laŭ la preskribo donita per ilia patro Aaron, kiel ordonis al li la Eternulo, Dio de Izrael.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
La ordo por la ceteraj idoj de Levi: el la idoj de Amram: Ŝubael; el la idoj de Ŝubael: Jeĥdeja;
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
ĉe Reĥabja: el la idoj de Reĥabja la unua estis Jiŝija;
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
ĉe la Jicharidoj: Ŝelomot; el la filoj de Ŝelomot: Jaĥat;
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
la filoj de Ĥebron: Jerija, Amarja estis la dua, Jaĥaziel la tria, Jekameam la kvara;
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
el la filoj de Uziel: Miĥa; el la filoj de Miĥa: Ŝamir;
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
la frato de Miĥa estis Jiŝija; el la filoj de Jiŝija: Zeĥarja;
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
el la filoj de Merari: Maĥli kaj Muŝi; el la filoj de Jaazija: Beno;
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
el la idoj de Merari: ĉe Jaazija: Beno, Ŝoham, Zakur, kaj Ibri;
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
ĉe Maĥli: Eleazar; li ne havis filojn;
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
ĉe Kiŝ: el la filoj de Kiŝ: Jeraĥmeel;
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
la filoj de Muŝi: Maĥli, Eder, kaj Jerimot. Tio estas la Levidoj laŭ iliaj patrodomoj.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
Ili ankaŭ lotis samtempe kun siaj fratoj la Aaronidoj, antaŭ la reĝo David, Cadok, Aĥimeleĥ, kaj la ĉefoj de patrodomoj de la pastroj kaj de la Levidoj: ĉefo de patrodomo egale kun sia pli malgranda frato.