< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
These are the groups of the descendants of Aaron [the first Supreme Priest]: Aaron’s four sons were Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abihu died before their father died, and they had no children. So their [younger] brothers Eleazar and Ithamar became the priests.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
Zadok, who was a descendant of Eleazar, and Ahimelech, who was a descendant of Ithamar, helped David to separate his descendants into two groups. Each group had certain duties.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
There were more leaders among the descendants of Eleazar than there were among the descendants of Ithamar. So they appointed 16 leaders from Eleazar’s descendants and eight leaders from Ithamar’s descendants.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
There were temple officials and priests, including descendants of both Eleazar and Ithamar, to make sure that the work was divided fairly. So they decided what work each person would do by (casting lots/throwing marked stones).
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Shemaiah, the son of Nethanel, who was a descendant of Levi, wrote down the names [of the leaders of each group] while David and his officials were watching. Zadok, the [Supreme] Priest, and Ahimelech [his assistant], and the leaders of the families of the priests and of the families of the other descendants of Levi also watched.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Jehoiarib was the first one whose name was selected [by casting lots/throwing marked stones]. Next Jedaiah was selected.
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
Next, Harim was selected. Next, Seorim was selected.
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
Next, Malkijah was selected. Next, Mijamin was selected.
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
Next, Hakkoz was selected. Next, Abijah was selected.
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
Next, Jeshua was selected. Next, Shecaniah was selected.
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
Next, Eliashib was selected. Next, Jakim was selected.
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
Next, Huppah was selected. Next, Jeshebeab was selected.
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
Next, Bilgah was selected. Next, Immer was selected.
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
Next, Hezir was selected. Next, Happizzez was selected.
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
Next, Pethahiah was selected. Next, Jehezkel was selected.
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
Next, Jakin was selected. Next, Gamul was selected.
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
Next, Delaiah was selected. Next, Maaziah was selected.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Those were the men who were chosen to be the leaders of the groups that would serve in the temple, obeying the regulations that were set down by Aaron, regulations which Yahweh, the God to whom the Israeli people belonged, had given to him.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
[This is a list of some of] the other descendants of Levi: Amram was the ancestor of Shubael and Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Rehabiah was the ancestor of Isshiah, the oldest son in his family.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Izhar was the father of Shelomoth and the grandfather of Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
[Kohath’s son] Hebron had four sons: Jeriah and his [younger] brothers Amariah, Jahaziel, and Jekameam.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Uzziel was the father of Micah and the grandfather of Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
Micah’s [younger] brother was the father of Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari were Mahli, Mushi, and Jaaziah.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
Jaaziah had four sons: Beno, Shoham, Zaccur, and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Mahli’s son Eleazar did not have any sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
From the descendants of [Mahli’s second son] there was Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons of Mushi were Mahli, Eder, and Jerimoth. Those were descendants of Levi who were listed according to the leaders of their families.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
The jobs they would do were decided by (casting lots/throwing marked stones), like their fellow Israelis, the descendants of Aaron, did. They cast lots {The lots were cast} while King David, Zadok, Ahimelech, and the leaders of the families of the priests and the [other] descendants of Levi watched. They gave the same jobs to the families of each oldest brother and each youngest brother.

< 1 Nyakati 24 >