< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
And the courses of the sons of Aaron were these. The sons of Aaron: Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abihu died before their father, and had no children; therefore Eleazar and Ithamar executed the priest's office.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
And David with Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, divided them according to their ordering in their service.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
And there were more chief men found of the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar; and thus were they divided: of the sons of Eleazar there were sixteen, heads of fathers' houses; and of the sons of Ithamar, according to their fathers' houses, eight.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
Thus were they divided by lot, one sort with another; for they were princes of the sanctuary and princes of God, both of the sons of Eleazar, and of the sons of Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
And Shemaiah the son of Nethanel the scribe, who was of the Levites, wrote them in the presence of the king, and the princes, and Zadok the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and the heads of the fathers' houses of the priests and of the Levites: one father's house being taken for Eleazar, and proportionately for Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Now the first lot came forth to Jehoiarib, the second to Jedaiah;
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
the third to Harim, the fourth to Seorim;
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin;
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah;
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah;
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim;
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab;
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer;
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez;
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel;
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
the one and twentieth to Jachin, the two and twentieth to Gamul;
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
the three and twentieth to Delaiah, the four and twentieth to Maaziah.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
These were the orderings of them in their service, to come into the house of the LORD according to the ordinance given unto them by the hand of Aaron their father, as the LORD, the God of Israel, had commanded him.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
And of the rest of the sons of Levi: of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Of Rehabiah: of the sons of Rehabiah, Isshiah the chief.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Of the Izharites, Shelomoth; of the sons of Shelomoth, Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
And Benai, Jeriah, Amariah the second, Jahaziel the third, Jekameam the fourth.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
The sons of Uzziel, Micah; of the sons of Micah, Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Micah, Isshiah; of the sons of Isshiah, Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi; the sons of Jaaziah, his son,
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
even the sons of Merari through Jaaziah his son: Shoham, and Zaccur, and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Of Mahli: Eleazar, who had no sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Of Kish: the sons of Kish, Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
And the sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites after their fathers' houses.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
These likewise cast lots even as their brethren the sons of Aaron in the presence of David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the heads of the fathers' houses of the priests and of the Levites; the fathers' houses of the chief even as those of his younger brother.

< 1 Nyakati 24 >