< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
The sons of Aaron were placed in divisions as follows. The sons of Aaron were Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abihu died before their father did, and they had no sons. Only Eleazar and Ithamar carried on as priests.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
With the help of Zadok, a descendant of Eleazar, and Ithamar, a descendant Ahimelech, David placed them in divisions according to their appointed duties.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Because Eleazar's descendants had more leaders than those of Ithamar, they were divided like this: sixteen family leaders from the descendants of Eleazar, and eight from the descendants of Ithamar.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
They were divided by casting lots, without preference, for there were officers of the sanctuary and officers of God from both the sons of Eleazar and the sons of Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
Shemaiah son of Nethanel, a Levite, was the secretary. He wrote down the names and assignments in the presence of the king, the officials, Zadok the priest, Ahimelech son of Abiathar, and the family leaders of the priests and Levites. One family from Eleazar and one from Ithamar were chosen in turn.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
The first lot fell to Jehoiarib. The second to Jedaiah.
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
The third to Harim. The fourth to Seorim.
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
The fifth to Malkijah. The sixth to Mijamin.
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
The seventh to Hakkoz. The eighth to Abijah.
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
The ninth to Jeshua. The tenth to Shecaniah.
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
The eleventh to Eliashib. The twelfth to Jakim.
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
The thirteenth to Huppah. The fourteenth to Jeshebeab.
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
The fifteenth to Bilgah. The sixteenth to Immer.
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
The seventeenth to Hezir. The eighteenth to Happizzez.
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
The nineteenth to Pethahiah. The twentieth to Jehezkel.
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
The twenty-first to Jakin. The twenty-second to Gamul.
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
The twenty-third to Delaiah. The twenty-fourth to Maaziah.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
This was the order in which each group were to serve when they came into the house of the Lord, following the procedure defined for them by their forefather Aaron, as instructed by the Lord, the God of Israel.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
These were the rest of the sons of Levi: from the sons of Amram: Shubael; from the sons of Shubael: Jehdeiah.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
For Rehabiah, from his sons: Isshiah (first).
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
From the Izharites: Shelomoth; from the sons of Shelomoth: Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
The sons of Hebron: Jeriah (first), Amariah (second), Jahaziel (third), and Jekameam (fourth).
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
The son of Uzziel: Micah; from the sons of Micah: Shamir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Micah: Isshiah; from the sons of Isshiah: Zechariah.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi. The son of Jaaziah: Beno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
The sons of Merari: from Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur and Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
From Mahli: Eleazar, who did not have any sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
From Kish: the son of Kish, Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons of Mushi: Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites, according to their families.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
They also cast lots in the same way their relatives the descendants of Aaron did. They did this in the presence of King David, and of Zadok, Ahimelech, and the family leaders of the priests and of the Levites, the family leaders and their youngest brothers alike.

< 1 Nyakati 24 >