< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Now these were the divisions of the sons of Aaron: The sons of Aaron: Nadab, and Abiu, and Eleazar, and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
But Nadab and Abiu died before their father, and had no children: so Eleazar, and Ithamar did the office of the priesthood.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
And David distributed them, that is, Sadoc of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, according to their courses and ministry.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
And there were found many more of the sons of Eleazar among the principal men, than of the sons of Ithamar. And he divided them so, that there were of the sons of Eleazar, sixteen chief men by their families: and of the sons of Ithamar eight by their families and houses.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
And he divided both the families one with the other by lot: for there were princes of the sanctuary, and princes of God, both of the sons of Eleazar, and of the sons of Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
And Semeias the son of Nathanael the scribe a Levite, wrote them down before the king and the princes, and Sadoc the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and the princes also of the priestly and Levitical families: one house, which was over the rest, of Eleazar: and another house, which had the rest under it, of Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Now the first lot came forth to Joiarib, the second to Jedei,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
The third to Harim, the fourth to Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
The fifth to Melchia, the sixth to Maiman,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
The seventh to Accos, the eighth to Abia,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
The ninth to Jesua, the tenth to Sechenia,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
The eleventh to Eliasib, the twelfth to Jacim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
The thirteenth to Hoppha, the fourteenth to Isbaab,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
The fifteenth to Belga, the sixteenth to Emmer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
The seventeenth to Hezir, the eighteenth to Aphses,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
The nineteenth to Pheteia, the twentieth to Hezechiel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
The one and twentieth to Jachin, the two and twentieth to Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
The three and twentieth to Dalaiau, the four and twentieth to Maaziau.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
These are their courses according to their ministries, to come into the house of the Lord, and according to their manner under the hand of Aaron their father: as the Lord the God of Israel had commanded.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Now of the rest of the sons of Levi, there was of the sons of Amram, Subael: and of the sons of Subael, Jehedeia.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Also of the sons of Rohobia the chief Jesias.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
And the son of Isaar Salemoth, and the son of Salemoth Jahath:
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
And his son Jeriau the first, Amarias the second, Jahaziel the third, Jecmaan the fourth.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
The son of Oziel, Micha: the son of Micha, Samir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
The brother of Micha, Jesia: and the son of Jesia, Zacharias.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
The sons of Merari: Moholi and Musi: the son of Oziau: Benno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
The son also of Merari: Oziau, and Seam, and Zacchur, and Hebri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
And the son of Moholi: Eleazar, who had no sons.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
And the son of Cis, Jeramael.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
The sons of Musi: Moholi, Eder, and Jerimoth. These are the sons of Levi according to the houses of their families.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
And they also cast lots over against their brethren the sons of Aaron before David the king, and Sadoc, and Ahimelech, and the princes of the priestly and Levitical families, both the elder and the younger. The lot divided all equally.