< 1 Nyakati 24 >
1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Aangaande nu de kinderen van Aaron, dit waren hun verdelingen. De zonen van Aaron waren Nadab, en Abihu, Eleazar en Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Maar Nadab stierf, en Abihu, voor het aangezicht huns vaders, en zij hadden geen kinderen. En Eleazar en Ithamar bedienden het priesterambt.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
David nu verdeelde hen, en Zadok uit de kinderen van Eleazar, en Abimelech uit de kinderen van Ithamar, naar hun ambt in hun dienst.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
En van de kinderen van Eleazar werden meer gevonden tot hoofden der mannen, dan van de kinderen van Ithamar, als zij hen afdeelden; van de kinderen van Eleazar waren zestien hoofden der vaderlijke huizen, maar van de kinderen van Ithamar, naar hun vaderlijke huizen, acht.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
En zij deelden hen door loten af, dezen met genen; want de oversten des heiligdoms en de oversten Gods waren uit de kinderen van Eleazar en van de kinderen van Ithamar.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
En Semaja, de zoon van Nethaneel, de schrijver, uit de Levieten, schreef hen op, voor het aangezicht des konings, en van de vorsten, en van den priester Zadok, en van Achimelech, den zoon van Abjathar, en van de hoofden der vaderen onder de priesters en onder de Levieten; een vaderlijk huis werd genomen voor Eleazar, en desgelijks werd genomen voor Ithamar.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Het eerste lot nu ging uit voor Jojarib, het tweede voor Jedaja,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
Het derde voor Harim, het vierde voor Seorim,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
Het vijfde voor Malchia, het zesde voor Mijamin,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
Het zevende voor Hakkoz, het achtste voor Abia,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
Het negende voor Jesua, het tiende voor Sechanja,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
Het elfde voor Eljasib, het twaalfde voor Jakim,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
Het dertiende voor Huppa, het veertiende voor Jesebeab,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
Het vijftiende voor Bilga, het zestiende voor Immer,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
Het zeventiende voor Hezir, het achttiende voor Happizzes,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
Het negentiende voor Petahja, het twintigste voor Jehezkel,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
Het een en twintigste voor Jachin, het twee en twintigste voor Gamul,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
Het drie en twintigste voor Delaja, het vier en twintigste voor Maazja.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Het ambt van dezen in hun dienst was te gaan in het huis des HEEREN, naar hun ordening door de hand van Aaron, huns vaders; gelijk als hem de HEERE, de God Israels, geboden had.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Van de overige kinderen van Levi nu, was van de kinderen van Amram Subael, van de kinderen van Subael was Jechdeja.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Aangaande Rehabja: van de kinderen van Rehabja was Jissia het hoofd.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Van de Jizharieten was Selomoth; van de kinderen van Selomoth was Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
En van de kinderen van Hebron was Jeria de eerste, Amarja de tweede, Jahaziel de derde, Jekameam de vierde.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Van de kinderen van Uzziel was Micha; van de kinderen van Micha was Samir;
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
De broeder van Micha was Jissia; van de kinderen van Jissia was Zecharja.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
De kinderen van Merari waren Maheli en Musi. De kinderen van Jaazia waren Beno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
De kinderen van Merari van Jaazia waren Beno, en Soham, en Zakkur, en Hibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Van Maheli was Eleazar; en die had geen kinderen.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Aangaande Kis: de kinderen van Kis waren Jerahmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
En de kinderen van Musi waren Maheli, en Eder, en Jeremoth. Dezen zijn de kinderen der Levieten, naar hun vaderlijke huizen.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
En zij wierpen ook loten, nevens hun broederen, de zonen van Aaron, voor het aangezicht van den koning David, en Zadok, en Achimelech, en van de hoofden der vaderen onder de priesteren en onder de Levieten; het hoofd der vaderen tegen zijn kleinsten broeder.