< 1 Nyakati 24 >

1 Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Synů pak Aronových tato jsou zpořádaní: Synové Aronovi: Nádab, Abiu, Eleazar a Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
Ale že umřel Nádab a Abiu před otcem svým, a neměli synů, protož konali úřad kněžský Eleazar a Itamar.
3 Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
Kteréž zpořádal David, totiž Sádocha z synů Eleazarových, a Achimelecha z synů Itamarových, vedlé počtu a řádu jejich v přisluhováních jejich.
4 Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
Nalezeno pak synů Eleazarových více předních mužů, než synů Itamarových, a rozdělili je. Z synů Eleazarových bylo předních po domích otcovských šestnáct, a z synů Itamarových po čeledech otcovských osm.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
I rozděleni jsou losem jedni od druhých, ačkoli byli knížata nad věcmi svatými, a knížata Boží z synů Eleazarových a z synů Itamarových.
6 Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
I popsal je Semaiáš syn Natanaelův, písař z pokolení Léví před králem a knížaty, a Sádochem knězem a Achimelechem synem Abiatarovým i knížaty čeledí otcovských mezi kněžími a Levíty, tak že dům otcovský jeden zaznamenán Eleazarovi, tolikéž druhý zaznamenán Itamarovi.
7 Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
Padl pak los první na Jehoiariba, na Jedaiáše druhý,
8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
Na Charima třetí, na Seorima čtvrtý,
9 ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
Na Malkiáše pátý, na Miamin šestý,
10 ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
Na Hakkoza sedmý, na Abiáše osmý,
11 ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
Na Jesua devátý, na Sechaniáše desátý,
12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
Na Eliasiba jedenáctý, na Jakima dvanáctý,
13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
Na Chuppa třináctý, na Jesebaba čtrnáctý,
14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
Na Bilgu patnáctý, na Immera šestnáctý,
15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
Na Chezira sedmnáctý, na Happizeza osmnáctý,
16 ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
Na Petachiáše devatenáctý, na Ezechiele dvadcátý,
17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
Na Jachina jedenmecítmý, na Gamule dvamecítmý,
18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
Na Delaiáše třimecítmý, na Maaseiáše čtyřmecítmý.
19 Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
Ti jsou, jenž zřízeni byli v přisluhováních svých, aby vcházeli do domu Hospodinova podlé řádu svého, pod spravou Arona otce jejich, jakož mu byl přikázal Hospodin Bůh Izraelský.
20 Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
Z synů Léví ostatních, z synů Amramových Subael, z synů Subael Jechdeiáš.
21 Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
Z Rechabiáše, z synů Rechabiášových kníže Iziáš.
22 Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
Z Izara Selomot, z synů Selomotových Jachat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
Synové pak Jeriášovi: Amariáš druhý, Jachaziel třetí, Jekamam čtvrtý.
24 Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
Syn Uzielův Mícha, z synů Míchy Samir.
25 Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
Bratr Míchův Iziáš, a syn Iziášův Zachariáš.
26 Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
Synové Merari: Moholi a Musi, synové Jaaziášovi: Beno.
27 Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
Synové Merari z Jaaziáše: Beno, Soham, Zakur a Ibri.
28 Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
Z Moholi Eleazar, kterýž neměl synů.
29 Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
Z Cisa synové Cisovi: Jerachmeel.
30 Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
Synové pak Musi: Moholi, Eder a Jerimot. Ti jsou synové Levítů po domích otců svých.
31 Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.
I ti také metali losy naproti bratřím svým, synům Aronovým, před Davidem králem, Sádochem a Achimelechem, i knížaty otcovských čeledí z kněží a Levítů, z čeledí otcovských, každý přednější naproti bratru svému mladšímu.

< 1 Nyakati 24 >