< 1 Nyakati 23 >
1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
Och när David blev gammal och levnadsmätt, gjorde han sin son Salomo till konung över Israel.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
Och han församlade alla Israels furstar, så ock prästerna och leviterna.
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
Och leviterna blevo räknade, de nämligen som voro trettio år gamla eller därutöver; och deras antal, antalet av alla personer av mankön, utgjorde trettioåtta tusen.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
»Av dessa», sade han, »skola tjugufyra tusen förestå sysslorna vid HERRENS hus, och sex tusen vara tillsyningsmän och domare;
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
fyra tusen skola vara dörrvaktare och fyra tusen skola lovsjunga HERREN till de instrumenter som jag har låtit göra för lovsången.»
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
Och David delade dem i avdelningar efter Levis söner, Gerson Kehat och Merari.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
Till gersoniterna hörde Laedan och Simei.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
Laedans söner voro Jehiel, huvudmannen, Setam och Joel, tillsammans tre.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
Simeis söner voro Selomot, Hasiel och Haran, tillsammans tre. Dessa voro huvudmän för Laedans familjer.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
Och Simeis söner voro Jahat, Sina, Jeus och Beria. Dessa voro Simeis söner, tillsammans fyra.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
Jahat var huvudmannen, och Sisa var den andre. Men Jeus och Beria hade icke många barn; därför fingo de utgöra allenast en familj, en ordning.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Kehats söner voro Amram, Jishar, Hebron och Ussiel, tillsammans fyra.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
Amrams söner voro Aron och Mose. Och Aron blev jämte sina söner för evärdlig tid avskild till att helgas såsom höghelig, till att för evärdlig tid antända rökelse inför HERREN och göra tjänst inför honom och välsigna i hans namn.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
Men gudsmannen Moses söner räknades till Levi stam.
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
Moses söner voro Gersom och Elieser.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
Gersoms söner voro Sebuel, huvudmannen.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
Och Eliesers söner voro Rehabja, huvudmannen. Elieser hade inga andra söner; men Rehabjas söner voro övermåttan talrika.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
Jishars söner voro Selomit, huvudmannen.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
Hebrons söner voro Jeria, huvudmannen, Amarja, den andre, Jahasiel, den tredje, och Jekameam, den fjärde.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
Ussiels söner voro Mika, huvudmannen, och Jissia, den andre.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
Meraris söner voro Maheli och Musi. Mahelis söner voro Eleasar och Kis.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
När Eleasar dog, lämnade han inga söner efter sig, utan allenast döttrar; men Kis' söner, deras fränder, togo dessa till hustrur.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
Musis söner voro Maheli, Eder och Jeremot, tillsammans tre.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
Dessa voro Levi barn, efter deras familjer, huvudmännen för familjerna, så många av dem som inmönstrades, vart namn räknat särskilt, var person för sig, de som kunde förrätta sysslor vid tjänstgöringen i HERRENS hus, nämligen de som voro tjugu år gamla eller därutöver.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
Ty David sade: »HERREN, Israels Gud, har låtit sitt folk komma till ro, och han har nu sin boning i Jerusalem till evig tid;
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
därför behöva icke heller leviterna mer bära tabernaklet och alla redskap till tjänstgöringen därvid.»
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
(Enligt berättelsen om Davids sista tid räknades nämligen av Levi barn de som voro tjugu år gamla eller därutöver.)
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
De fingo i stället sin plats vid Arons söners sida för tjänstgöringen i HERRENS hus, i vad som rörde förgårdarna och kamrarna och reningen av allt heligt och sysslorna vid tjänstgöringen i Guds hus,
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
vare sig det gällde skådebröden eller det fina mjölet till spisoffret eller de osyrade tunnkakorna eller plåtarna eller det hopknådade mjölet, eller något mått och mål,
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
eller att var morgon göra tjänst genom att tacka och lova HERREN, och likaledes var afton,
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
eller att offra alla brännoffer åt HERREN på sabbaterna, vid nymånaderna och vid högtiderna, till bestämt antal och såsom det var föreskrivet för dem, beständigt, inför HERRENS ansikte.
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
De skulle iakttaga vad som var att iakttaga vid uppenbarelsetältet och vid det heliga, vad Arons söner, deras bröder, hade att iakttaga vid tjänstgöringen i HERRENS hus.