< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
Un kad Dāvids bija vecs un savu laiku nodzīvojis, tad tas savu dēlu Salamanu cēla par ķēniņu pār Israēli.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
Un (Dāvids) sapulcēja visus Israēla virsniekus un priesterus un Levitus.
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
Un Leviti tapa skaitīti no trīsdesmit gadiem un pārāk, un viņu skaits pēc viņu vīru galvām bija trīsdesmit astoņi tūkstoši.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
No tiem bija divdesmit četri tūkstoši nolikti pie Tā Kunga nama darba, un seši tūkstoš uzraugi un tiesneši.
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
Un četri tūkstoš vārtu sargi un četri tūkstoš Tā Kunga dziedātāji ar spēlēm, ko es esmu iecēlis, Dievu teikt (sacīja Dāvids).
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
Un Dāvids tos dalīja kārtās, pēc Levja bērniem, Geršona, Kehāta un Merarus.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
No Geršona bērniem bija Laēdans un Šimejus.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
Laēdana bērni bija: Jeīels, virsnieks, un Zetams un Joēls, tie trīs.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
Šimejus bērni bija: Zalomits un Aziēls un Hārans, tie trīs; šie bija Laēdana tēvu nama virsnieki.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
Un Šimejus bērni bija: Jakats, Zinus un Jeūs un Brija; šie četri bija Šimejus bērni.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
Un Jakats bija pirmais un Zinus otrais. Bet Jeūm un Brijam nebija daudz bērnu, tāpēc tie tapa skaitīti par vienu tēva namu.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Un Kehāta bērni bija: Amrams, Jecears, Hebrons un Uziēls, tie četri.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
Amrama bērni bija Ārons un Mozus. Un Āronu atšķīra, ka tas taptu svētīts visusvētākajā amatā līdz ar saviem dēliem mūžīgi, kvēpināt priekš Tā Kunga vaiga un viņam kalpot un svētīt viņa vārdā mūžīgi.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
Un Mozus, Tā Dieva vīra, bērni bija skaitīti pie Levitu cilts.
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
Mozus bērni bija: Ģerzoms un Eliēzers.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
Ģerzoma bērni bija Zebuēls, virsnieks.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
Un Eliēzeram bērni bija: Rekabeja, virsnieks. Un Eliēzeram nebija citu bērnu. Bet Rekabejas bērni vairojās daudz vairāk.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
Jeceara bērni bija: virsnieks Zalomits.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
Hebrona bērni bija: Jerija tas pirmais, Amarija otrais, Jeaziēls trešais, un Jakmeams ceturtais.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
Uziēļa bērni bija: Miha tas pirmais un Jezija otrais.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
Merarus bērni bija: Maēlus un Muzus. Maēlus bērni bija: Eleazars un Ķis.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
Un Eleazars nomira, un tam dēlu nebija, bet meitas vien, un Ķisa bērni, viņu brāļi, tās apņēma.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
Muzus bērni bija Maēlns, Eders un Jeremots, tie trīs.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
Šie bija Levja bērni pēc savu tēvu namiem, savu tēvu namu virsnieki, kas pēc vārdiem tapa skaitīti pēc viņu galvām; tie stāvēja kalpošanas darbā Tā Kunga namā, divdesmit gadus veci un vairāk.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
Jo Dāvids bija sacījis: Tas Kungs, Israēla Dievs, Saviem ļaudīm dusu devis, un Viņš Jeruzālemē mājos mūžīgi.
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
Tad arī Levitiem vairs nebija jānes tas dzīvoklis, nedz kādas citas lietas, kas pie tā amata piederēja.
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
Bet pēc Dāvida pēdējiem vārdiem Levja bērni tapa skaitīti, divdesmit gadus veci un vairāk,
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
Ka tiem bija jāstāv apakš Ārona bērnu rokas, kalpot Tā Kunga nama pagalmā un mantas kambaros un tīrīt visas svētās lietas un stāvēt Dieva nama kalpošanā,
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
Un pie Dieva priekšā noliekamām maizēm un ēdamo upuru kviešu miltiem un neraudzētām karašām un pannām un ceptiem raušiem un pie visiem svariem un mēriem,
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
Un ik rītu stāvēt, To Kungu teikt un slavēt, tāpat arī ik vakaru,
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
Un upurēt visus dedzināmos upurus svētdienās, jaunos mēnešos un svētkos pēc sava skaita un tiesas Tā Kunga priekšā vienmēr,
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
Un sargāt saiešanas telti un svēto vietu un kalpot saviem brāļiem, Ārona bērniem, Tā Kunga nama kalpošanā.

< 1 Nyakati 23 >