< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
David donc, vieux et plein de jours, établit Salomon, son fils, roi sur Israël.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
Et il assembla tous les princes d’Israël, et les prêtres et les Lévites.
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
Et les Lévites furent dénombrés depuis trente ans et au-dessus, et il s’en trouva trente-huit mille.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
On en choisit et on en distribua, pour le service de la maison du Seigneur, vingt-quatre mille; mais les gouverneurs et les juges étaient au nombre de six mille.
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
Il y avait aussi quatre mille portiers et autant de joueurs de psaltérion, chantant les louanges du Seigneur sur les instruments que David avait faits pour chanter.
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
Et David les distribua selon les classes des fils de Lévi; savoir: Gerson, Caath et Mérari.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
Les fils de Gerson étaient Léédan et Séméi.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
Les fils de Léédan: le prince Jahiel, Zéthan et Joël; trois.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
Les fils de Séméi: Salomith, Hosiel et Aran, trois. Ce sont là les princes des familles de Léédan.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
Et les fils de Séméi: Léheth, Ziza, Jaüs et Baria. Ce sont là les fils de Séméi, quatre.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
Léheth était donc le premier, Ziza le second: or Jaüs et Baria n’eurent pas beaucoup d’enfants; c’est pourquoi ils furent comptés comme une seule famille et une seule maison.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Les fils de Caath: Amram, Isaar, Hébron et Oziel, quatre.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
Les fils d’Amram: Aaron et Moïse. Or Aaron fut séparé pour servir dans le Saint des saints, lui et ses enfants à jamais, et pour offrir l’encens au Seigneur selon son rite, et pour bénir son nom perpétuellement.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
Les enfants de Moïse, l’homme de Dieu, furent aussi comptés dans la tribu de Lévi.
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
Les fils de Moïse furent Gersom et Eliézer.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
Les fils de Gersom: Subuel, le premier.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
Or les fils d’Eliézer furent Rohobia, le premier; et Eliézer n’eut point d’autres fils; mais les fils de Rohobia se multiplièrent extrêmement.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
Les fils d’Isaar: Salomith, le premier.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
Les fils d’Hébron: Jériaü, le premier; Amarias, le second; Jahaziel, le troisième; Jecmaam, le quatrième.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
Les fils d’Oziel: Micha, le premier, et Jésia, le second.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
Les fils de Mérari: Moholi et Musi. Les fils de Moholi: Eléazar et Cis.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
Or Eléazar mourut et n’eut pas de fils, mais des filles; et les fils de Cis, leur frères, les épousèrent.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
Les fils de Musi furent Moholi, Eder et Jérimoth, trois.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
Ce sont là les fils de Lévi selon leur parenté et leurs familles, princes, qui, à leur tour, et suivant le dénombrement qui en avait été fait, tête par tête, accomplissaient les œuvres du ministère de la maison du Seigneur, depuis vingt ans et au-dessus.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
Car David dit: Le Seigneur Dieu d’Israël a donné le repos à son peuple, et l’habitation de Jérusalem à jamais.
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
Il ne sera pas de l’office des Lévites de porter désormais le tabernacle, et tous ses vases destinés au ministère.
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
C’est aussi selon les dernières ordonnances de David que sera compté le nombre des enfants de Lévi, depuis vingt ans et au-dessus.
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
Et ils seront sous la main des fils d’Aaron pour le culte de la maison du Seigneur, dans les vestibules, dans les chambres, dans le lieu de la purification, dans le sanctuaire, et dans toutes les œuvres du ministère du temple du Seigneur.
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
Mais les prêtres auront l’intendance sur les pains de proposition, sur le sacrifice de fleur de farine, sur les beignets azymes, sur la poêle, sur ce qui doit être rôti, et sur tous les poids et toutes les mesures.
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
Quant aux lévites, qu’ils soient prêts le matin à louer et à chanter le Seigneur, et également le soir,
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
Tant à l’oblation des holocaustes du Seigneur qu’aux jours de sabbat, aux calendes et autres solennités, selon le nombre et les cérémonies prescrites pour chaque chose; qu’ils soient continuellement devant le Seigneur.
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
Qu’ils aient soin de garder le tabernacle d’alliance, le rite du sanctuaire, et le respect envers les enfants d’Aaron, leurs frères, pour remplir leur ministère dans la maison du Seigneur.

< 1 Nyakati 23 >