< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
David, âgé et rassasié de jours, établit Salomon, son fils, roi sur Israël.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
Il assembla tous les chefs d’Israël, les sacrificateurs et les Lévites.
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
On fit le dénombrement des Lévites, depuis l’âge de trente ans et au-dessus; comptés par tête et par homme, ils se trouvèrent au nombre de trente-huit mille.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
Et David dit: Qu’il y en ait vingt-quatre mille pour veiller aux offices de la maison de l’Éternel, six mille comme magistrats et juges,
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
quatre mille comme portiers, et quatre mille chargés de louer l’Éternel avec les instruments que j’ai faits pour le célébrer.
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
David les divisa en classes d’après les fils de Lévi, Guerschon, Kehath et Merari.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
Des Guerschonites: Laedan et Schimeï.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
Fils de Laedan: le chef Jehiel, Zétham et Joël, trois.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
Fils de Schimeï: Schelomith, Haziel et Haran, trois. Ce sont là les chefs des maisons paternelles de la famille de Laedan.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
Fils de Schimeï: Jachath, Zina, Jeusch et Beria. Ce sont là les quatre fils de Schimeï.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
Jachath était le chef, et Zina le second; Jeusch et Beria n’eurent pas beaucoup de fils, et ils formèrent une seule maison paternelle dans le dénombrement.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Fils de Kehath: Amram, Jitsehar, Hébron et Uziel, quatre.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
Fils d’Amram: Aaron et Moïse. Aaron fut mis à part pour être sanctifié comme très saint, lui et ses fils à perpétuité, pour offrir les parfums devant l’Éternel, pour faire son service, et pour bénir à toujours en son nom.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
Mais les fils de Moïse, homme de Dieu, furent comptés dans la tribu de Lévi.
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
Fils de Moïse: Guerschom et Éliézer.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
Fils de Guerschom: Schebuel, le chef.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
Et les fils d’Éliézer furent: Rechabia, le chef; Éliézer n’eut pas d’autre fils, mais les fils de Rechabia furent très nombreux.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
Fils de Jitsehar: Schelomith, le chef.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
Fils d’Hébron: Jerija, le chef; Amaria, le second; Jachaziel, le troisième; et Jekameam, le quatrième.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
Fils d’Uziel: Michée, le chef; et Jischija, le second.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
Fils de Merari: Machli et Muschi. Fils de Machli: Éléazar et Kis.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
Éléazar mourut sans avoir de fils; mais il eut des filles, que prirent pour femmes les fils de Kis, leurs frères.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
Fils de Muschi: Machli, Éder et Jerémoth, trois.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
Ce sont là les fils de Lévi, selon leurs maisons paternelles, les chefs des maisons paternelles, d’après le dénombrement qu’on en fit en comptant les noms par tête. Ils étaient employés au service de la maison de l’Éternel, depuis l’âge de vingt ans et au-dessus.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
Car David dit: L’Éternel, le Dieu d’Israël, a donné du repos à son peuple, et il habitera pour toujours à Jérusalem;
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
et les Lévites n’auront plus à porter le tabernacle et tous les ustensiles pour son service.
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
Ce fut d’après les derniers ordres de David qu’eut lieu le dénombrement des fils de Lévi depuis l’âge de vingt ans et au-dessus.
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
Placés auprès des fils d’Aaron pour le service de la maison de l’Éternel, ils avaient à prendre soin des parvis et des chambres, de la purification de toutes les choses saintes, des ouvrages concernant le service de la maison de Dieu,
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
des pains de proposition, de la fleur de farine pour les offrandes, des galettes sans levain, des gâteaux cuits sur la plaque et des gâteaux frits, de toutes les mesures de capacité et de longueur:
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
ils avaient à se présenter chaque matin et chaque soir, afin de louer et de célébrer l’Éternel,
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
et à offrir continuellement devant l’Éternel tous les holocaustes à l’Éternel, aux sabbats, aux nouvelles lunes et aux fêtes, selon le nombre et les usages prescrits.
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
Ils donnaient leurs soins à la tente d’assignation, au sanctuaire, et aux fils d’Aaron, leurs frères, pour le service de la maison de l’Éternel.

< 1 Nyakati 23 >