< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
and David be old and to satisfy day and to reign [obj] Solomon son: child his upon Israel
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
and to gather [obj] all ruler Israel and [the] priest and [the] Levi
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
and to recount [the] Levi from son: aged thirty year and above [to] and to be number their to/for head their to/for great man thirty and eight thousand
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
from these to/for to conduct upon work house: temple LORD twenty and four thousand and official and to judge six thousand
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
and four thousand gatekeeper and four thousand to boast: praise to/for LORD in/on/with article/utensil which to make to/for to boast: praise
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
and to divide them David division to/for son: child Levi to/for Gershon Kohath and Merari
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
to/for Gershonite Ladan and Shimei
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
son: child Ladan [the] head: leader Jehiel and Zetham and Joel three
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
son: child Shimei (Shelomoth *Q(K)*) and Haziel and Haran three these head: leader [the] father to/for Ladan
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
and son: child Shimei Jahath Zizah and Jeush and Beriah these son: child Shimei four
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
and to be Jahath [the] head: leader and Zizah [the] second and Jeush and Beriah not to multiply son: child and to be to/for house: household father to/for punishment one
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
son: child Kohath Amram Izhar Hebron and Uzziel four
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
son: descendant/people Amram Aaron and Moses and to separate Aaron to/for to consecrate: dedicate him holiness holiness he/she/it and son: descendant/people his till forever: enduring to/for to offer: offer to/for face: before LORD to/for to minister him and to/for to bless in/on/with name his till forever: enduring
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
and Moses man [the] God son: child his to call: call by upon tribe [the] Levi
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
son: child Moses Gershom and Eliezer
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
son: descendant/people Gershom Shebuel [the] head: leader
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
and to be son: descendant/people Eliezer Rehabiah [the] head: leader and not to be to/for Eliezer son: child another and son: child Rehabiah to multiply to/for above [to]
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
son: child Izhar Shelomith [the] head: leader
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
son: child Hebron Jeriah [the] head: leader Amariah [the] second Jahaziel [the] third and Jekameam [the] fourth
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
son: child Uzziel Micah [the] head: leader and Isshiah [the] second
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
son: child Merari Mahli and Mushi son: child Mahli Eleazar and Kish
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
and to die Eleazar and not to be to/for him son: child that if: except if: except daughter and to lift: marry them son: child Kish brother: male-relative their
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
son: child Mushi Mahli and Eder and Jerimoth three
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
these son: child Levi to/for house: household father their head: leader [the] father to/for to reckon: list their in/on/with number name to/for head their to make: do [the] work to/for service: ministry house: temple LORD from son: aged twenty year and above [to]
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
for to say David to rest LORD God Israel to/for people his and to dwell in/on/with Jerusalem till to/for forever: enduring
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
and also to/for Levi nothing to/for to lift: bear [obj] [the] tabernacle and [obj] all article/utensil his to/for service: ministry his
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
for in/on/with word David [the] last they(masc.) number son: aged Levi from son: aged twenty year and to/for above [to]
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
for office their to/for hand: to son: descendant/people Aaron to/for service: ministry house: temple LORD upon [the] court and upon [the] chamber and upon purifying to/for all holiness and deed: work service: ministry house: temple [the] God
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
and to/for food: bread [the] row and to/for fine flour to/for offering and to/for flatbread [the] unleavened bread and to/for griddle and to/for to stir and to/for all capacity and measure
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
and to/for to stand: stand in/on/with morning in/on/with morning to/for to give thanks and to/for to boast: praise to/for LORD and so to/for evening
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
and to/for all to ascend: offer up burnt offering to/for LORD to/for Sabbath to/for month: new moon and to/for meeting: festival in/on/with number like/as justice: rule upon them continually to/for face: before LORD
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
and to keep: obey [obj] charge tent meeting and [obj] charge [the] holiness and charge son: descendant/people Aaron brother: male-relative their to/for service: ministry house: temple LORD

< 1 Nyakati 23 >