< 1 Nyakati 23 >
1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
And David he was old and he was satisfied days and he made king Solomon son his over Israel.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
And he gathered all [the] leaders of Israel and the priests and the Levites.
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
And they were counted the Levites from a son of thirty year[s] and up-wards and it was number their to skulls their to men thirty and eight thousand.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
From these [are] to act as overseers over [the] work of [the] house of Yahweh twenty and four thousand and officials and judges six thousand.
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
And four thousand gatekeepers and four thousand [those] praising Yahweh with instruments which I made to praise.
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
And he divided them David divisions. [the] sons of Levi to Gershon Kohath and Merari.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
Of the Gershonite[s] Ladan and Shimei.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
[the] sons of Ladan the chief Jehiel and Zetham and Joel three.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
[the] sons of Shimei (Shelomith *Q(K)*) and Haziel and Haran three these [were] [the] heads of the fathers of Ladan.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
And [the] sons of Shimei Jahath Zina and Jeush and Beriah these [were] [the] sons of Shimei four.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
And he was Jahath the chief and Zizah the second and Jeush and Beriah not they had many sons and they became a house of a father a group one.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
[the] sons of Kohath Amram Izhar Hebron and Uzziel four.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
[the] sons of Amram Aaron and Moses and he was separated Aaron to consecrate it a holy one of holy ones he and descendants his until perpetuity to make smoke before Yahweh to serve him and to bless in name his until perpetuity.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
And Moses [the] man of God descendants his they were named on [the] tribe of the Levite[s].
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
[the] sons of Moses Gershom and Eliezer.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
[the] sons of Gershom Shebuel the chief.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
And they were [the] sons of Eliezer Rehabiah the chief and not it belonged to Eliezer sons other and [the] sons of Rehabiah they were numerous upwards.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
[the] sons of Izhar Shelomith the chief.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
[the] sons of Hebron Jeriah the chief Amariah the second Jahaziel the third and Jekameam the fourth.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
[the] sons of Uzziel Micah the chief and Isshiah the second.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
[the] sons of Merari Mahli and Mushi [the] sons of Mahli Eleazar and Kish.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
And he died Eleazar and not they belonged to him sons that except daughters and they took them [the] sons of Kish relatives their.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
[the] sons of Mushi Mahli and Eder and Jeremoth three.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
These [were] [the] descendants of Levi to [the] house of ancestors their [the] chiefs of the fathers to [men] enrolled their by number of names to skulls their doer[s] of the work of [the] service of [the] house of Yahweh from a son of twenty year[s] and up-wards.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
For he had said David he has given rest Yahweh [the] God of Israel to people his and he has settled in Jerusalem until for ever.
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
And also to the Levites there not [is] to carry the tabernacle and all articles its for service its.
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
For by [the] words of David last they [were] [the] number of [the] descendants of Levi from a son of twenty year[s] and upwards.
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
For function their [was] to [the] side of [the] descendants of Aaron for [the] service of [the] house of Yahweh over the courts and over the store-rooms and over [the] purification of every holy thing and [the] work of [the] service of [the] house of God.
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
And to [the] bread of the row and to fine flour for a grain offering and to [the] wafers of the unleavened bread and to the baked cake and to the mixed [dough] and to every measurement and measurement.
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
And to stand in the morning in the morning to give thanks and to praise Yahweh and thus to the evening.
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
And to every of ering up of burnt offerings to Yahweh for the sabbaths for the new moons and for the appointed feasts by number according to [the] ordinance on them continually before Yahweh.
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
And they kept [the] duty of [the] tent of meeting and [the] duty of the holy place and [the] duty of [the] descendants of Aaron relatives their for [the] service of [the] house of Yahweh.