< 1 Nyakati 22 >
1 Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
Potem je David rekel: »To je hiša Gospoda Boga in to je oltar žgalne daritve za Izraela.«
2 Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
David je zapovedal, da zberejo skupaj tujce, ki so bili v Izraelovi deželi in postavil je zidarje, da izklesajo kamne, da zgradijo Božjo hišo.
3 Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
David je pripravil železa v obilju za žeblje za duri velikih vrat in za vezi in brona v obilju, brez teže.
4 Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
Tudi cedrovih dreves v obilju, kajti Sidónci in tisti iz Tira so Davidu prinesli veliko cedrovega lesa.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
David je rekel: »Moj sin Salomon je mlad in nežen, hiša, ki naj se zgradi za Gospoda, pa mora biti silno prekrasna od slovesa in od slave po vseh deželah, zato bom torej naredil priprave zanjo.« Tako je David pred svojo smrtjo [vsega] obilno pripravil.
6 Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
Potem je dal poklicati svojega sina Salomona in ga zadolžil, da zgradi hišo za Gospoda, Izraelovega Boga.
7 Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
David je rekel Salomonu: »Moj sin, kar se mene tiče, je bilo v mojih mislih, da zgradim hišo imenu Gospoda, svojega Boga,
8 Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
toda k meni je prišla Gospodova beseda, rekoč: ›Obilno si prelival kri in storil velike vojne. Ne boš gradil hiše mojemu imenu, ker si v mojem pogledu na zemlji prelil mnogo krvi.
9 Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
Glej, rojen ti bo sin, ki bo mož počitka in dal mu bom počitek pred vsemi njegovimi sovražniki naokoli, kajti njegovo ime bo Salomon in jaz bom v njegovih dneh Izraelu dal mir in spokojnost.
10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
Zgradil bo hišo za moje ime in on bo moj sin in jaz bom njegov oče in jaz bom vzpostavil prestol njegovega kraljestva nad Izraelom na veke.‹
11 “Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
Sedaj moj sin, Gospod naj bo s teboj in bodi uspešen in zgradi hišo Gospoda, svojega Boga, kakor je govoril o tebi.
12 Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
Samo Gospod naj ti da modrost in razumevanje in te zadolži glede Izraela, da se boš lahko držal postave Gospoda, svojega Boga.
13 Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
Potem boš uspel, če paziš, da izpolnjuješ zakone in sodbe, ki jih je Gospod zapovedal Mojzesu glede Izraela. Bodi močan in odločnega poguma. Ne boj se niti ne bodi zaprepaden.
14 “Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
Torej glej, v svoji stiski sem za Gospodovo hišo pripravil sto tisoč talentov zlata in milijon talentov srebra, brona in železa pa brez teže, kajti tega je v obilju. Tudi les in kamenje sem pripravil in ti lahko k temu dodaš.
15 Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
Poleg tega je tam s teboj delavcev v obilju, kamnosekov in obdelovalcev kamna in lesa, in vseh vrst spretnih mož za vsako vrsto dela.
16 wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
Zlatu, srebru, bronu in železu ni števila. Vstani torej in delaj in Gospod naj bo s teboj.«
17 Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
David je tudi vsem Izraelovim princem zapovedal, da pomagajo njegovemu sinu Salomonu, rekoč:
18 Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
» Mar ni z vami Gospod, vaš Bog? In ali vam ni dal počitka na vsaki strani? Kajti prebivalce dežele je izročil v mojo roko in dežela je podjarmljena pred Gospodom in pred njegovim ljudstvom.
19 Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”
Pripravite torej svoje srce in svojo dušo, da iščete Gospoda, svojega Boga. Vstanite torej in zgradite svetišče Gospodu Bogu, da se prinese skrinja Gospodove zaveze in svete Božje posode v hišo, ki naj bo zgrajena Gospodovemu imenu.«