< 1 Nyakati 22 >

1 Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
Et David dit: C'est ici la maison du Seigneur, et voici l'autel des holocaustes pour Israël.
2 Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
Puis, il ordonna de réunir tous les étrangers qui se trouvaient en la terre d'Israël, et il chargea des tailleurs de pierres de tailler des pierres, pour bâtir la maison de Dieu.
3 Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
Et David prépara beaucoup de fer, des clous pour les portes et leurs vantaux, des gonds et une quantité d'airain d'un poids incalculable,
4 Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
Et un nombre infini de cèdres que les Tyriens et les Sidoniens lui apportèrent.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
Et David dit: Mon fils Salomon est d'âge tendre, et la maison qui doit être bâtie au Seigneur surpassera en magnificence, en renom et en gloire, toutes celles de la terre; je préparerai tout pour cela. Et David fit ses apprêts à profusion avant de mourir.
6 Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
Et il appela Salomon, son fils, et il lui ordonna de bâtir le temple du Seigneur Dieu d'Israël.
7 Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
Et David dit à Salomon: Enfant, mon âme a voulu bâtir un temple au nom du Seigneur Dieu.
8 Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
Mais la parole du Seigneur est venue à moi, disant: Tu as versé beaucoup de sang, tu as fait de grandes guerres; tu ne bâtiras point un temple à mon nom, parce que, devant moi, tu as répandu beaucoup de sang sur cette terre.
9 Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
Voici qu'un fils t'est né; celui-là sera un homme de paix, et je le maintiendrai en paix avec tous les ennemis qui l'entourent; car son nom est Salomon, et j'accorderai, pendant sa vie, le repos et la paix à Israël.
10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
C'est lui qui bâtira un temple à mon nom, et il sera pour moi un fils, et moi je serai pour lui un père, et je dresserai son trône royal en Israël pour toujours.
11 “Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
Maintenant, mon fils, le Seigneur sera avec toi; il te fera prospérer, et tu bâtiras le temple du Seigneur ton Dieu, comme il me l'a fait savoir.
12 Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
Que le Seigneur te donne seulement l'intelligence et la sagesse, et il t'affermira sur Israël, pour que tu observes et que tu mettes en pratique la loi du Seigneur ton Dieu.
13 Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
Alors, il te fera prospérer, si tu veilles à observer les commandements et les préceptes que le Seigneur a donnés au peuple par la voix de Moïse. Sois fort, et agis en homme; n'aie ni crainte ni faiblesse.
14 “Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
Vois, dans ma pauvreté, j'ai préparé pour la maison du Seigneur: cent mille talents d'or, un million de talents d'argent, de l'airain et du fer en telle abondance, qu'on n'en peut dire le compte. J'ai aussi préparé des bois et des pierres, et tu y ajouteras encore,
15 Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
Et tu t'adjoindras une multitude d'ouvriers, artisans, tailleurs de pierres, charpentiers, et tout homme habile à mettre en œuvre
16 wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
L'or, l'argent, et une masse innombrable d'airain et de fer. Courage donc, et agis, le Seigneur sera avec toi.
17 Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
Ensuite, David ordonna à tous les chefs d'Israël de seconder Salomon, son fils, et il leur dit:
18 Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
Le Seigneur n'est-il pas avec vous? Il vous a donné le repos tout alentour; il vous a livré ceux qui habitaient la terre promise, et la terre s'est soumise devant le Seigneur et devant son peuple.
19 Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”
Appliquez-vous donc, cœur et âme, à chercher le Seigneur, excitez-vous, et bâtissez pour votre Dieu un lieu saint, afin d'y transporter l'arche de l'alliance du Seigneur, avec les vases et les ornements consacrés à Dieu, qui résideront dans le temple élevé au nom du Seigneur.

< 1 Nyakati 22 >