< 1 Nyakati 22 >
1 Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
Et David dit: « Voici la maison de Yahvé Dieu, et voici l'autel des holocaustes pour Israël. »
2 Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
David donna l'ordre de rassembler les étrangers qui se trouvaient dans le pays d'Israël, et il chargea des maçons de tailler des pierres de taille pour construire la maison de Dieu.
3 Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
David prépara du fer en abondance pour les clous des portes et pour les assemblages, du bronze en abondance et sans poids,
4 Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
et des cèdres en abondance, car les Sidoniens et les habitants de Tyr avaient apporté à David des cèdres en abondance.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
David dit: « Salomon, mon fils, est jeune et tendre, et la maison que l'on va bâtir pour Yahvé doit être d'une grande splendeur, renommée et glorieuse dans tous les pays. Je vais donc la préparer. » David fit donc d'abondants préparatifs avant sa mort.
6 Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
Puis il appela Salomon, son fils, et lui ordonna de construire une maison pour Yahvé, le Dieu d'Israël.
7 Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
David dit à Salomon, son fils: « Quant à moi, j'avais à cœur de bâtir une maison au nom de l'Éternel, mon Dieu.
8 Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
Mais la parole de l'Éternel m'a été adressée en ces termes: « Tu as versé beaucoup de sang et tu as fait de grandes guerres. Tu ne bâtiras pas une maison à mon nom, parce que tu as versé beaucoup de sang sur la terre, sous mes yeux.
9 Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
Voici qu'il te naîtra un fils, qui sera un homme de paix. Je lui donnerai du repos contre tous ses ennemis d'alentour, car son nom sera Salomon, et je donnerai la paix et le calme à Israël en ses jours.
10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
Il bâtira une maison à mon nom; il sera mon fils, et je serai son père; et j'affermirai le trône de son royaume sur Israël pour toujours'.
11 “Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
Maintenant, mon fils, que Yahvé soit avec toi et te fasse prospérer, et que tu bâtisses la maison de Yahvé ton Dieu, comme il l'a dit à ton sujet.
12 Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
Que l'Éternel te donne du discernement et de l'intelligence, et qu'il te mette à la tête d'Israël, afin que tu observes la loi de l'Éternel, ton Dieu.
13 Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
Tu prospéreras alors, si tu observes et mets en pratique les lois et les ordonnances que l'Éternel a données à Moïse concernant Israël. Sois fort et courageux. N'aie pas peur et ne t'effraie pas.
14 “Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
Voici, dans ma détresse, j'ai préparé pour la maison de l'Éternel cent mille talents d'or, un million de talents d'argent, du bronze et du fer sans poids, car il y en a en abondance. J'ai aussi préparé du bois et de la pierre, et tu pourras y ajouter.
15 Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
Il y a aussi avec toi des ouvriers en abondance, des tailleurs de pierre et de bois, et toutes sortes d'hommes habiles dans toutes sortes d'ouvrages;
16 wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
pour l'or, l'argent, le bronze et le fer, il n'y a pas de nombre. Lève-toi et agis, et que Yahvé soit avec toi. »
17 Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
David ordonna aussi à tous les princes d'Israël d'aider Salomon, son fils, en disant:
18 Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
« Yahvé, ton Dieu, n'est-il pas avec toi? Ne t'a-t-il pas donné du repos de tous côtés? Car il a livré entre mes mains les habitants du pays, et le pays est soumis à Yahvé et à son peuple.
19 Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”
Maintenant, mets ton cœur et ton âme à la suite de l'Éternel, ton Dieu. Lève-toi donc, et bâtis le sanctuaire de Yahvé Dieu, pour faire entrer l'arche de l'alliance de Yahvé et les vases sacrés de Dieu dans la maison qui doit être bâtie au nom de Yahvé. »