< 1 Nyakati 22 >

1 Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
And Dauid seide, This is the hows of God, and this auter is in to brent sacrifice of Israel.
2 Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
And he comaundide that alle conuersis fro hethenesse to the lawe of Israel `schulden be gaderid `of the lond of Israel; and he ordeynede of hem masouns for to kytte stoonys and for to polische, that the hows of the Lord schulde be bildid;
3 Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
also Dauid made redy ful myche yrun to the nailes of the yatis, and to the medlyngis and ioyntouris, and vnnoumbrable weiyte of bras;
4 Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
also the trees of cedre myyten not be gessid, whiche the men of Sidonye and the men of Tyre brouyten to Dauid.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
And Dauid seide, Salomon, my sone, is a litil child and delicat; sotheli the hows, which Y wole be bildid to the Lord, owith to be sich, that it be named in alle cuntrees; therfor Y schal make redi necessaries to hym. And for this cause Dauid bifor his deeth made redi alle costis.
6 Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
And he clepide Salomon, his sone, and comaundide to hym, that he schulde bilde an hows to the Lord God of Israel.
7 Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
And Dauid seide to Salomon, My sone, it was my wille to bilde an hows to the name of `my Lord God;
8 Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
but the word of the Lord was made to me, and seide, Thou hast sched out myche blood, and thou hast fouyt ful many batels; thou mayst not bilde an hows to my name, for thou hast sched out so myche blood bifor me;
9 Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
the sone that schal be borun to thee, schal be a man most pesible, for Y schal make hym to haue reste of alle hise enemyes bi cumpas, and for this cause he schal be clepid pesible, and Y schal yyue pees and reste in Israel in alle hise daies.
10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
He schal bilde an hows to my name; he schal be to me in to a sone, and Y schal be to hym in to a fadir, and Y schal make stidefast the seete of his rewme on Israel withouten ende.
11 “Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
Now therfor, my sone, the Lord be with thee, and haue thou prosperite, and bilde thou an hows to `thi Lord God, as he spak of thee.
12 Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
And the Lord yyue to thee prudence and wit, that thou mow gouerne Israel, and kepe the lawe of `thi Lord God.
13 Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
For thanne thou maist profite, if thou kepist the comaundementis and domes, whiche the Lord comaundide to Moises, that he schulde teche Israel; be thou coumfortid, and do manli, drede thou not `with outforth, nether drede thou `with ynne.
14 “Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
Lo! in my pouert Y haue maad redi the costis of the hows of the Lord; an hundrid thousinde talentis of gold, and a thousynde thousynde talentis of siluer; sotheli of bras and irun is no weiyte, for the noumbre is ouercomun bi greetnesse; Y haue maad redi trees and stoonys to alle costis.
15 Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
Also thou hast ful many crafti men, masouns, and leggeris of stonys, and crafti men of trees, and of alle craftis,
16 wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
most prudent to make werk, in gold, and siluer, and bras, and in yrun, of which is no noumbre; therfor rise thou, and make, and the Lord schal be with thee.
17 Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
Also Dauid comaundide to alle the princis of Israel, that thei schulden helpe Salomon,
18 Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
his sone, and seide, Ye seen, that `youre Lord God is with you, and hath youe to you reste `by cumpas, and hath bitake alle enemyes in youre hoond, and the erthe is suget bifor the Lord, and bifor his puple.
19 Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”
Therfor yyue youre hertis and youre soulis, that ye seke `youre Lord God; and rise ye togidere, and bilde ye a seyntuarie to `youre Lord God, that the arke of boond of pees of the Lord be brouyt in, and that vessels halewid to the Lord be brouyt in to the hows, which is bildid to the name of the Lord.

< 1 Nyakati 22 >