< 1 Nyakati 22 >

1 Ndipo Daudi akasema, “Nyumba ya Bwana Mungu itakuwa mahali hapa, pia pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Israeli.”
I řekl David: Totoť jest místo domu Hospodina Boha, a toto jest místo oltáři k zápalu Izraelovi.
2 Kwa hiyo Daudi akatoa amri wakusanyike wageni wote waliokuwa wanaishi Israeli, na kutoka miongoni mwao akaweka waashi ili kuchonga mawe kwa ajili ya kujenga nyumba ya Mungu.
Protož přikázal David, aby shromáždili cizozemce přebývající v zemi Izraelské, a ustanovil z nich kameníky, aby tesali kamení k stavení domu Božího.
3 Daudi akatoa chuma tele ili kutengenezea misumari kwa ajili ya mafungo ya malango ya nyumba na shaba tele isiyopimika.
Železa také mnoho na hřeby, a na dvéře k branám i k spojováním, připravil David, i mědi mnoho bez váhy.
4 Pia akatoa magogo ya mierezi yasiyohesabika, kwa kuwa Wasidoni na Watiro walikuwa wamemletea Daudi idadi kubwa ya mierezi.
Též i dříví cedrového bez počtu; nebo přiváželi Sidonští a Tyrští dříví cedrového množství Davidovi.
5 Daudi akasema, “Mwanangu Solomoni bado ni mdogo wa umri na hana uzoefu. Nyumba itakayojengwa kwa ajili ya Bwana inatakiwa iwe yenye uzuri mwingi na sifa na fahari mbele ya mataifa yote. Kwa hiyo nitaifanyia matayarisho.” Daudi akafanya matayarisho makubwa kabla ya kifo chake.
Nebo řekl byl David: Šalomoun syn můj mládenček jest malý, dům pak vystaven býti má Hospodinu veliký, znamenitý a slovoutný po všech zemích, a protož připravím mu nyní potřeb. A tak připravil David množství toho před smrtí svou.
6 Kisha akamwita Solomoni mwanawe akamwagiza kujenga nyumba kwa ajili ya Bwana, Mungu wa Israeli.
Potom povolav Šalomouna syna svého, přikázal mu, aby vystavěl dům Hospodinu Bohu Izraelskému.
7 Daudi akamwambia Solomoni: “Mwanangu, nilikuwa na jambo hili ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wangu.
A řekl David Šalomounovi: Synu můj, uložil jsem byl v srdci svém vystavěti dům jménu Hospodina Boha svého.
8 Lakini neno hili la Bwana likanijia, kusema: ‘Wewe umemwaga damu nyingi na kupigana vita vingi. Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu.
Ale stala se ke mně řeč Hospodinova, řkoucí: Mnohou jsi krev vylil, a boje veliké jsi vedl; nebudeš stavěti domu jménu mému, proto že jsi mnoho krve vylil na zem přede mnou.
9 Lakini utakuwa na mwana ambaye atakuwa mtu wa amani na utulivu nami nitampa utulivu mbele ya adui zake wote pande zote. Jina lake ataitwa Solomoni, nami nitawapa Israeli amani na utulivu wakati wa utawala wake.
Aj, syn narodí se tobě, tenť bude muž pokojný. Odpočinutí zajisté dám jemu vůkol přede všemi nepřátely jeho, pročež Šalomoun slouti bude; nebo pokoj a odpočinutí dám Izraelovi za dnů jeho.
10 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu. Yeye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake. Nami nitakifanya imara kiti chake cha enzi cha utawala wake katika Israeli milele.’
Onť ustaví dům jménu mému, a on bude mi za syna, a já jemu za otce, a upevním trůn království jeho nad Izraelem až na věky.
11 “Sasa, mwanangu, Bwana awe pamoja nawe, nawe uwe na mafanikio upate kuijenga nyumba ya Bwana Mungu wako, kama alivyosema utafanya.
Protož, synu můj, Hospodin bude s tebou, a šťastněť se povede, a vystavíš dům Hospodina Boha svého, jakož mluvil o tobě.
12 Bwana na akupe hekima na ufahamu wakati atakuweka juu ya Israeli, ili uweze kuishika sheria ya Bwana Mungu wako.
A však dejž tobě Hospodin rozum a moudrost, a ustanoviž tě nad Izraelem, abys ostříhal zákona Hospodina Boha svého.
13 Ndipo utakapofanikiwa, ikiwa utakuwa na bidii kutii amri na sheria Bwana alizompa Mose kwa ajili ya Israeli. Uwe hodari na ushujaa. Usiogope wala usikate tamaa.
A tehdyť se šťastně povede, když ostříhati a činiti budeš ustanovení a soudy, kteréž přikázal Hospodin skrze Mojžíše lidu Izraelskému. Posilniž se a zmocni, neboj se, ani lekej.
14 “Nimejitaabisha sana ili kupata mahitaji kwa ajili ya Hekalu la Bwana: talanta 100,000 za dhahabu, talanta 1,000,000 za fedha na kiasi kisichopimika cha shaba na chuma, pia mbao na mawe. Nawe waweza kuviongeza.
A aj, já v nevolech svých připravil jsem k domu Hospodinovu sto tisíců centnéřů zlata, a stříbra tisíc tisíců centnéřů, mědi pak a železa bez váhy; nebo toho mnoho jest. Dříví také i kamení připravil jsem, a k tomu ostatek přidáš.
15 Unao wafanyakazi wengi: Wachonga mawe, waashi na maseremala, pamoja na watu walio na ustadi katika kila kazi
Přes to máš u sebe hojně dělníků, kameníků a zedníků, i tesařů i jiných zběhlých ve všelijakém díle.
16 wa kufua dhahabu, fedha, shaba na chuma, mafundi wasiohesabika. Sasa basi anza kazi hii, naye Bwana awe pamoja nawe.”
Zlata, stříbra, mědi a železa není počtu; snažiž se a dělej, a Hospodin budiž s tebou.
17 Kisha Daudi akawaamuru viongozi wote wa Israeli wamsaidie Solomoni mwanawe.
Přikázal také David všechněm knížatům Izraelským, aby pomáhali Šalomounovi synu jeho, řka:
18 Akawaambia, “Je, Bwana Mungu wenu si yuko pamoja na ninyi? Pia si amewapa raha pande zote? Kwa maana amewatia wenyeji wa nchi mkononi mwangu, nayo nchi iko chini ya Bwana na watu wake.
Zdaliž Hospodin Bůh váš není s vámi, kterýž vám způsobil vůkol a vůkol odpočinutí? Nebo dal v ruku mou obyvatele země této, a podmaněna jest země Hospodinu a lidu jeho.
19 Sasa itoeni mioyo yenu na nafsi zenu katika kumtafuta Bwana Mungu wenu. Anzeni kujenga Maskani ya Bwana Mungu, ili mweze kulileta Sanduku la Agano la Bwana na vyombo vitakatifu vya Mungu katika Hekalu litakalojengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.”
Nyní tedy vydejte se srdcem svým a duší svou k hledání Hospodina Boha svého, a přičiníce se, vystavějte svatyni Hospodinu Bohu, abyste tam vnesli truhlu smlouvy Hospodinovy, a nádobí Bohu posvěcená do domu vystaveného jménu Hospodinovu.

< 1 Nyakati 22 >