< 1 Nyakati 21 >

1 Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
and to stand: stand Satan upon Israel and to incite [obj] David to/for to count [obj] Israel
2 Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
and to say David to(wards) Joab and to(wards) ruler [the] people: soldiers to go: went to recount [obj] Israel from Beersheba Beersheba and till Dan and to come (in): bring to(wards) me and to know [obj] number their
3 Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
and to say Joab to add LORD upon people his like/as them hundred beat not lord my [the] king all their to/for lord my to/for servant/slave to/for what? to seek this lord my to/for what? to be to/for guiltiness to/for Israel
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
and word [the] king to strengthen: prevail over upon Joab and to come out: come Joab and to go: went in/on/with all Israel and to come (in): come Jerusalem
5 Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
and to give: give Joab [obj] number appointment [the] people to(wards) David and to be all Israel thousand thousand and hundred thousand man to draw sword and Judah four hundred and seventy thousand man to draw sword
6 Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
and Levi and Benjamin not to reckon: list in/on/with midst their for to abhor word [the] king with Joab
7 Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
and be evil in/on/with eye: appearance [the] God upon [the] word: thing [the] this and to smite [obj] Israel
8 Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
and to say David to(wards) [the] God to sin much which to make: do [obj] [the] word: thing [the] this and now to pass please [obj] iniquity: crime servant/slave your for be foolish much
9 Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
and to speak: speak LORD to(wards) Gad seer David to/for to say
10 “Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
to go: went and to speak: speak to(wards) David to/for to say thus to say LORD three I to stretch upon you to choose to/for you one from them and to make: do to/for you
11 Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
and to come (in): come Gad to(wards) David and to say to/for him thus to say LORD to receive to/for you
12 miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
if three year famine and if three month to snatch from face: before enemy your and sword enemy your to/for to overtake and if three day sword LORD and pestilence in/on/with land: country/planet and messenger: angel LORD to ruin in/on/with all border: area Israel and now to see: select what? to return: return [obj] to send: depart me word: speaking
13 Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
and to say David to(wards) Gad distress to/for me much to fall: fall please in/on/with hand: power LORD for many compassion his much and in/on/with hand: power man not to fall: fall
14 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
and to give: give LORD pestilence in/on/with Israel and to fall: kill from Israel seventy thousand man
15 Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
and to send: depart [the] God messenger: angel to/for Jerusalem to/for to ruin her and like/as to ruin to see: see LORD and to be sorry: relent upon [the] distress: harm and to say to/for messenger: angel [the] to ruin many now to slacken hand: power your and messenger: angel LORD to stand: stand with threshing floor Ornan [the] Jebusite
16 Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
and to lift: look David [obj] eye his and to see: see [obj] messenger: angel LORD to stand: stand between [the] land: country/planet and between [the] heaven and sword his to draw in/on/with hand his to stretch upon Jerusalem and to fall: fall David and [the] old: elder to cover in/on/with sackcloth upon face their
17 Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
and to say David to(wards) [the] God not I to say to/for to count in/on/with people and I he/she/it ([the] to pasture *X*) which to sin and be evil be evil and these [the] flock what? to make: do LORD God my to be please hand: power your in/on/with me and in/on/with house: household father my and in/on/with people your not to/for plague
18 Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
and messenger: angel LORD to say to(wards) Gad to/for to say to/for David for to ascend: rise David to/for to arise: raise altar to/for LORD in/on/with threshing floor Ornan [the] Jebusite
19 Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
and to ascend: rise David in/on/with word Gad which to speak: speak in/on/with name LORD
20 Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
and to return: return Ornan and to see: see [obj] [the] messenger: angel and four son: child his with him to hide and Ornan to tread wheat
21 Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
and to come (in): come David till Ornan and to look Ornan and to see: see [obj] David and to come out: come from [the] threshing floor and to bow to/for David face land: soil [to]
22 Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
and to say David to(wards) Ornan to give: give [emph?] to/for me place [the] threshing floor and to build in/on/with him altar to/for LORD in/on/with silver: price full to give: give him to/for me and to restrain [the] plague from upon [the] people
23 Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
and to say Ornan to(wards) David to take: take to/for you and to make: do lord my [the] king [the] pleasant in/on/with eye: appearance his to see: behold! to give: give [the] cattle to/for burnt offering and [the] threshing sled to/for tree: wood and [the] wheat to/for offering [the] all to give: give
24 Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
and to say [the] king David to/for Ornan not for to buy to buy in/on/with silver: price full for not to lift: raise which to/for you to/for LORD and to ascend: offer up burnt offering for nothing
25 Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
and to give: pay David to/for Ornan in/on/with place shekel gold weight six hundred
26 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
and to build there David altar to/for LORD and to ascend: offer up burnt offering and peace offering and to call: call to to(wards) LORD and to answer him in/on/with fire from [the] heaven upon altar [the] burnt offering
27 Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
and to say LORD to/for messenger: angel and to return: return sword his to(wards) sheath her
28 Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
in/on/with time [the] he/she/it in/on/with to see: see David for to answer him LORD in/on/with threshing floor Ornan [the] Jebusite and to sacrifice there
29 Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
and tabernacle LORD which to make Moses in/on/with wilderness and altar [the] burnt offering in/on/with time [the] he/she/it in/on/with high place in/on/with Gibeon
30 Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.
and not be able David to/for to go: went to/for face: before his to/for to seek God for to terrify from face of sword messenger: angel LORD

< 1 Nyakati 21 >