< 1 Nyakati 20 >
1 Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
Et à l'époque du retour de l'année, à l'époque de la mise en campagne des rois, Joab conduisit la force armée, et ravagea le pays des Ammonites et vint mettre le siège devant Rabba. Cependant David resta à Jérusalem. Et Joab vint à bout de Rabba et la détruisit.
2 Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
Et David prit la couronne de leur roi de dessus sa tête, et la trouva pesant un talent d'or et garnie de pierres précieuses, et il la posa sur sa propre tête, et il tira dehors le butin de la ville en immense quantité.
3 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
Et il la fit évacuer par le peuple qui l'habitait, et les hacha avec des scies et des traîneaux ferrés et des cognées. Et David en fit autant à toutes les villes des Ammonites. Puis David avec tout son monde revint à Jérusalem.
4 Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
Et dans la suite il y eut hostilité à Gézer avec les Philistins. Alors Sibkaï, de Husta, battit Sippaï, l'un des enfants nés à Rapha, et les Philistins furent abaissés.
5 Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Et il y eut encore hostilité avec les Philistins. Alors Elchanan, fils de Jaïs, battit Lachemi, frère de Goliath, de Gath. Or la hampe de sa lance était comme une ensuble de tisserand.
6 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Et il y eut de nouveau hostilité à Gath. Là était un homme de haute stature, qui avait six doigts et six orteils, vingt-quatre. Lui aussi était des enfants nés à Rapha.
7 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Et il défia Israël. Et Jonathan, fils de Simea, frère de David, le battit.
8 Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ces hommes étaient nés à Rapha à Gath, et ils périrent par la main de David et par la main de ses serviteurs.