< 1 Nyakati 20 >

1 Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
Le cours de l'année ramena le temps où les rois se mettent en campagne. Joab emmena toutes les forces de l'armée, et il ravagea la contrée des fils d'Ammon; il assiégea ensuite Rhabba, pendant que David était resté à Jérusalem; Joab prit Rhabba (Rabbath), et la détruisit.
2 Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
Et David prit sur la tête du roi Molchom sa couronne, qui pesait un talent d'or, et qui était ornée de pierres précieuses; elle allait à la tête de David; enfin, il rapporta de cette ville un immense butin.
3 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
Et il emmena tout le peuple qui l'habitait, et il l'extermina en plaçant les uns sous des scies, les autres sous des haches de fer, d'autres sous la cognée du bûcheron. Ce fut ainsi que David traita tous les fils d'Ammon, et David et tout le peuple retournèrent à Jérusalem.
4 Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
Ensuite, la guerre recommença avec les Philistins de Gazer. Alors, Sobochaï le Sasathite tua Saphut, de la race des géants, après l'avoir humilié.
5 Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Et il y eut une autre guerre avec les Philistins; et Eléanan, fils de Jaïr, tua Lachmi, frère de Goliath de Geth, qui portait une lance comme le mât d'un tisserand.
6 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Et il y eut encore une guerre avec Geth. Or, il y avait un homme de grande taille, issu des géants, et qui avait vingt-quatre doigts, six à chaque main, et six à chaque pied.
7 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Et il insulta Israël; et Jonathas, dis de Semas, frère de David, le tua. Ces hommes étaient de la race de Rhapha de Geth.
8 Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ils étaient quatre, tous géants, et ils tombèrent sous les coups de David et de ses serviteurs.

< 1 Nyakati 20 >