< 1 Nyakati 20 >

1 Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
Et il arriva, au temps du retour de l’année, au temps où les rois entrent en campagne, que Joab conduisit le gros de l’armée, et dévasta le pays des fils d’Ammon; et il vint et assiégea Rabba; mais David resta à Jérusalem. Et Joab frappa Rabba et la détruisit.
2 Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
Et David prit la couronne de leur roi de dessus sa tête (or elle fut trouvée du poids d’un talent d’or, et il y avait dessus des pierres précieuses); et elle fut [mise] sur la tête de David; et il emmena de la ville une grande quantité de butin.
3 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
Et il fit sortir le peuple qui s’y trouvait, et les scia avec la scie, et avec des herses de fer, et avec des scies: et David fit ainsi à toutes les villes des fils d’Ammon. Et David et tout le peuple s’en retournèrent à Jérusalem.
4 Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
Et il arriva, après cela, qu’il y eut un combat à Guézer avec les Philistins. Alors Sibbecaï, le Hushathite, frappa Sippaï [qui était] d’entre les enfants du géant; et ils furent subjugués.
5 Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Et il y eut encore un combat avec les Philistins: et Elkhanan, fils de Jaïr, frappa Lakhmi, frère de Goliath, le Guitthien; et le bois de sa lance était comme l’ensouple des tisserands.
6 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Et il y eut encore un combat à Gath: et il y avait [là] un homme de haute stature qui avait six doigts et six [orteils], [en tout] 24; et lui aussi était né au géant.
7 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Et il outragea Israël; mais Jonathan, fils de Shimha, frère de David, le frappa.
8 Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ceux-là étaient nés au géant, à Gath, et tombèrent par la main de David et par la main de ses serviteurs.

< 1 Nyakati 20 >