< 1 Nyakati 20 >

1 Mwanzoni mwa mwaka mpya, wakati ambapo wafalme huenda vitani, Yoabu aliliongoza jeshi. Aliangamiza nchi ya Waamoni, na akaenda Raba na kuuzingira, lakini Daudi alibaki Yerusalemu. Yoabu akashambulia Raba na kuuacha ukiwa magofu.
In spring, at the time of year when kings go out to make war, Joab led the Israelite army in attacks against the country of the Ammonites, also besieging Rabbah. However, David remained behind in Jerusalem. Joab attacked Rabbah and destroyed it.
2 Daudi akachukua taji kutoka kwa kichwa cha mfalme wao, lililokuwa na uzito wa talanta moja ya dhahabu, nayo ilizungushiwa vito vya thamani. Ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Alichukua nyara nyingi kutoka mjini huo.
David took the crown from the head of their idol Milcom. It was made of gold, and was set with gems. It weighed a talent and was placed on David's head. David also took a great deal of plunder from the city.
3 Akawatoa watu waliokuwa humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, sululu za chuma na mashoka. Daudi akafanya hivi kwa miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na jeshi lake lote wakarudi Yerusalemu.
David made the people there work with saws, iron picks, and axes. He also did the same to all the Ammonite towns. Then David and all his army returned to Jerusalem.
4 Baada ya muda, kulitokea vita dhidi ya Wafilisti, huko Gezeri. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Sipai, aliyekuwa mmoja wa wazao wa Warefai, nao Wafilisti wakashindwa.
Some time after this was broke out with the Philistines at Gezer. But then Sibbecai the Hushathite killed Sippai, a descendant of the Rephaim, and the Philistines were forced to submit.
5 Katika vita vingine na Wafilisti, Elhanani mwana wa Yairi alimuua Lahmi nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
In another battle with the Philistines, Elhanan, son of Jair, killed Lahmi, the brother of Goliath the Gittite. The shaft of his spear was as thick as a weaver's rod.
6 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu: jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
In yet another battle at Gath, there was a gigantic man, who had six fingers on each hand and six toes on each foot, making twenty-four all. He too was descended from the giants.
7 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani, mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
But when he insulted Israel, Jonathan, son of Shimea, David's brother, killed him.
8 Hawa walikuwa ndio wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
These were the descendants of the giants in Gath, abut they were all killed by David and his men.

< 1 Nyakati 20 >