< 1 Nyakati 2 >
1 Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
Éstos son los hijos de Israel: Rubén, Simeón, Leví, Judá, Isacar, Zabulón,
2 Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
Dan, José, Benjamín, Neftalí, Gad y Aser.
3 Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
Hijos de Judá: Er, Onán y Sela. Estos tres le nacieron de la hija de Súa, cananea. Pero Er, primogénito de Judá, fue perverso ante Yavé, Quien lo mató.
4 Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
Tamar su nuera le dio a luz a Fares y a Zera. Todos los hijos de Judá fueron cinco.
5 Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
Hijos de Fares: Hezrón y Hamul.
6 Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
Hijos de Zera: Zimri, Etán, Hemán, Calcol y Dara. Todos los hijos de Judá fueron cinco.
7 Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
Hijo de Carmi fue Acán, perturbador de Israel, porque transgredió en cuanto a lo maldito.
8 Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
Hijo de Etán: Azarías.
9 Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
Los hijos que le nacieron a Hezrón: Jerameel, Ram y Quelubai.
10 Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
Ram engendró a Aminadab, y Aminadab engendró a Naasón, jefe de los hijos de Judá.
11 Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
Naasón engendró a Salmón, y Salmón engendró a Booz.
12 Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
Booz engendró a Obed, y Obed engendró a Isaí.
13 Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
Isaí engendró a Eliab su primogénito, el segundo Abinadab, el tercero Simea,
14 wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
el cuarto Natanael, el quinto Radai,
15 wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
el sexto Ozem, el séptimo David,
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
de los cuales Sarvia y Abigail fueron hermanas. Los hijos de Sarvia fueron tres: Abisai, Joab y Asael.
17 Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
Abigail dio a luz a Amasa, cuyo padre fue Jeter ismaelita.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
Caleb, hijo de Hezrón, engendró a Jeriot de su esposa Azuba. Los hijos de ella fueron Jeser, Sobab y Ardón.
19 Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
Al morir Azuba, Caleb tomó como esposa a Efrata, la cual dio a luz a Hur.
20 Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
Hur engendró a Uri, y Uri a Bezaleel.
21 Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
Después Hezrón se unió a la hija de Maquir, padre de Galaad, a la cual tomó cuando él tenía 60 años, y ella dio a luz a Segub.
22 Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
Segub engendró a Jaír, quien poseyó 23 ciudades en la tierra de Galaad.
23 (Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
Pero Gesur y Aram tomaron las aldeas de Jaír, y Kenat y sus aldeas: 60 pueblos. Todas éstas las tomaron los hijos de Maquir, padre de Galaad.
24 Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
Después que Hezrón murió en Caleb-efrata, Abías, esposa de Hezrón, dio a luz a Asur, padre de Tecoa.
25 Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
Los hijos de Jerameel, primogénito de Hezrón, fueron: Ram, su primogénito, Buna, Orén, Ozem y Ahías.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
Jerameel tuvo otra mujer llamada Atara, que fue madre de Onam.
27 Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
Hijos de Ram, primogénito de Jerameel: Maaz, Jamín y Equer.
28 Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
Hijos de Onam: Samai y Jada. Hijos de Samai: Nadab y Abisur.
29 Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
El nombre de la esposa de Abisur fue Abihail, la cual dio a luz a Ahbán y a Molid.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
Hijos de Nadab: Seled y Apaim. Seled murió sin hijos.
31 Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
Isi fue hijo de Apaim, y Sesán, hijo de Isi, e hijo de Sesán, Ahlai.
32 Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
Hijos de Jada, hermano de Samai: Jeter y Jonatán. Jeter murió sin hijos.
33 Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
Hijos de Jonatán: Pelet y Zaza. Tales fueron los descendientes de Jerameel.
34 Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
Sesán no tuvo hijos, sino hijas. Pero Sesán tenía un esclavo egipcio llamado Jarha.
35 Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
A éste, Sesán dio su hija como esposa, y ella dio a luz a Atai.
36 Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
Atai engendró a Natán, Natán a Zabad,
37 Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
Zabad a Eflal, Eflal a Obed,
38 Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
Obed a Jehú, Jehú a Azarías,
39 Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
Azarías a Heles, Heles a Elasa,
40 Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
Elasa a Sismai, Sismai a Salum,
41 Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
Salum a Jecamías, y Jecamías a Elisama.
42 Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
Hijos de Caleb, hermano de Jerameel: Mesa su primogénito, que fue el padre de Zif, y los hijos de Maresa, padre de Hebrón.
43 Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
Hijos de Hebrón: Coré, Tapúa, Requem y Sema.
44 Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
Sema engendró a Raham, padre de Jorcoam, y Requem engendró a Samai.
45 Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
Maón fue hijo de Samai, y Maón padre de Bet-sur.
46 Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
Efa, concubina de Caleb, dio a luz a Harán, Mosa y Gazez. Harán engendró a Gazez.
47 Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
Hijos de Jahdai: Regem, Jotam, Gesam, Pelet, Efa y Saaf.
48 Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
Maaca, concubina de Caleb, dio a luz a Seber y Tirhana.
49 Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
También dio a luz a Saaf, padre de Madmana, y a Seva, padre de Macbena, y padre de Gibea; y Acsa fue hija de Caleb.
50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
Éstos fueron los hijos de Caleb: hijos de Hur, primogénito de Efrata: Sobal, padre de Quiriat-jearim,
51 Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
Salma, padre de Belén, y Haref, padre de Bet-gader.
52 Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
Hijos de Sobal, padre de Quiriat-jearim: Haroe, la mitad de los manahetitas.
53 pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
Familias de Quiriat-jearim: los itritas, los futitas, los sumatitas y los misraítas, de los cuales salieron los zoratitas y los estaolitas.
54 Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
Hijos de Salma: Belén, y los netofatitas, Atrot-beth-joab, y Hazi-hammanahti, zoraíta.
55 pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.
Las familias de los escribas que habitaban en Jabes: los tirateos, los simeateos y los sucateos, los cuales son los ceneos, que proceden de Hamat, padre de la casa de Recab.