< 1 Nyakati 2 >
1 Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
filii autem Israhel Ruben Symeon Levi Iuda Isachar et Zabulon
2 Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
Dan Ioseph Beniamin Nepthali Gad Aser
3 Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
filii Iuda Her Aunan Sela tres nati sunt ei de filia Sue Chananitidis fuit autem Her primogenitus Iuda malus coram Domino et occidit eum
4 Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
Thamar autem nurus eius peperit ei Phares et Zara omnes ergo filii Iuda quinque
5 Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
filii autem Phares Esrom et Hamul
6 Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
filii quoque Zarae Zamri et Ethan et Eman Chalchal quoque et Darda simul quinque
7 Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
filii Carmi Achar qui turbavit Israhel et peccavit in furto anathematis
8 Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
filii Ethan Azarias
9 Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
filii autem Esrom qui nati sunt ei Ieremahel et Ram et Chalubi
10 Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
porro Ram genuit Aminadab Aminadab autem genuit Naasson principem filiorum Iuda
11 Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
Naasson quoque genuit Salma de quo ortus est Boez
12 Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
Boez vero genuit Obed qui et ipse genuit Isai
13 Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
Isai autem genuit primogenitum Heliab secundum Abinadab tertium Samaa
14 wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
quartum Nathanahel quintum Raddai
15 wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
sextum Asom septimum David
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
quorum sorores fuerunt Sarvia et Abigail filii Sarviae Abisai Ioab et Asahel tres
17 Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
Abigail autem genuit Amasa cuius pater fuit Iether Ismahelites
18 Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
Chaleb vero filius Esrom accepit uxorem nomine Azuba de qua genuit Ierioth fueruntque filii eius Iesar et Sobab et Ardon
19 Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
cumque mortua fuisset Azuba accepit uxorem Chaleb Ephrath quae peperit ei Ur
20 Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
porro Ur genuit Uri et Uri genuit Beselehel
21 Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
post haec ingressus est Esrom ad filiam Machir patris Galaad et accepit eam cum esset annorum sexaginta quae peperit ei Segub
22 Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
sed et Segub genuit Iair et possedit viginti tres civitates in terra Galaad
23 (Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
cepitque Gessur et Aram oppida Iair et Canath et viculos eius sexaginta civitatum omnes isti filii Machir patris Galaad
24 Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
cum autem mortuus esset Esrom ingressus est Chaleb ad Ephrata habuit quoque Esrom uxorem Abia quae peperit ei Assur patrem Thecue
25 Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
nati sunt autem filii Hieramehel primogeniti Esrom Ram primogenitus eius et Buna et Aran et Asom et Ahia
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
duxit quoque uxorem alteram Hieramehel nomine Atara quae fuit mater Onam
27 Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
sed et filii Ram primogeniti Hieramehel fuerunt Moos et Iamin et Achar
28 Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
Onam autem habuit filios Semmei et Iada filii autem Semmei Nadab et Abisur
29 Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
nomen vero uxoris Abisur Abiail quae peperit Ahobban et Molid
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
filii autem Nadab fuerunt Saled et Apphaim mortuus est autem Saled absque liberis
31 Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
filius vero Apphaim Iesi qui Iesi genuit Sesan porro Sesan genuit Oholi
32 Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
filii autem Iada fratris Semmei Iether et Ionathan sed et Iether mortuus est absque liberis
33 Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
porro Ionathan genuit Phaleth et Ziza isti fuerunt filii Hieramehel
34 Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
Sesan autem non habuit filios sed filias et servum aegyptium nomine Ieraa
35 Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
deditque ei filiam suam uxorem quae peperit ei Eththei
36 Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
Eththei autem genuit Nathan et Nathan genuit Zabad
37 Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
Zabad quoque genuit Ophlal et Ophlal genuit Obed
38 Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
Obed genuit Ieu Ieu genuit Azariam
39 Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
Azarias genuit Helles Helles genuit Elasa
40 Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
Elasa genuit Sisamoi Sisamoi genuit Sellum
41 Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
Sellum genuit Icamian Icamian genuit Elisama
42 Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
filii autem Chaleb fratris Hieramehel Mosa primogenitus eius ipse est pater Ziph et filii Maresa patris Hebron
43 Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
porro filii Hebron Core et Thapphu et Recem et Samma
44 Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
Samma autem genuit Raam patrem Iercaam et Recem genuit Semmei
45 Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
filius Semmei Maon et Maon pater Bethsur
46 Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
Epha autem concubina Chaleb peperit Arran et Musa et Gezez porro Arran genuit Gezez
47 Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
filii Iadai Regom et Iotham et Gesum et Phaleth et Epha et Saaph
48 Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
concubina Chaleb Maacha peperit Saber et Tharana
49 Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
genuit autem Saaph pater Madmena Sue patrem Machbena et patrem Gabaa filia vero Chaleb fuit Achsa
50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
hii erant filii Chaleb filii Ur primogeniti Ephrata Sobal pater Cariathiarim
51 Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
Salma pater Bethleem Ariph pater Bethgader
52 Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
fuerunt autem filii Sobal patris Cariathiarim qui videbat dimidium requietionum
53 pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
et de cognatione Cariathiarim Iethrei et Apphutei et Semathei et Maserei ex his egressi sunt Saraitae et Esthaolitae
54 Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
filii Salma Bethleem et Netophathi coronae domus Ioab et dimidium requietionis Sarai
55 pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.
cognationes quoque scribarum habitantium in Iabis canentes atque resonantes et in tabernaculis commorantes hii sunt Cinei qui venerunt de calore patris domus Rechab