< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
Isarel imthung hateh Reuben, Simeon, Levih, Judah, Issakhar hoi Zebulun,
2 Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
Dan, Joseph, Benjamin, Naphtali, Gad hoi Asher.
3 Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
Judah casaknaw teh: Er, Onan hoi Shelah. Hate kathum touh teh Kanaan napui Bathshua hoi a sak e naw doeh. Er teh Judah e camin lah ao ei, BAWIPA mithmu vah tamikathout lah ao dawkvah a due sak.
4 Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
A langa Tamar ni hai ahni hanlah Perez hoi Zerah a khe pouh dawkvah, Judah casak heh abuemlah panga touh a pha awh.
5 Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
Perez casaknaw teh: Khetsron hoi Hamul.
6 Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
Zerah casaknaw teh: Zimri, Ethan, Heman, Khalkol hoi Dara hoi abuemlah panga touh a pha awh.
7 Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
Karmi casak teh Akhar doeh. Isarelnaw runae ka poe e, thoebo e ka parawt e Akhan doeh.
8 Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
Ethan casak Azariah.
9 Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
Khetsron casak Jerahmeel ni ahni hanlah Ram hoi Khelubai a sak pouh.
10 Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
Ram ni Amminadab a sak. Amminadab ni Judah casak khobawi Nahshon a sak.
11 Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
Nahshon ni Salma hah a sak teh Salma ni Boaz hah a sak.
12 Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
Boaz ni Obed a sak teh Obed ni Jesi a sak.
13 Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
Jesi ni a camin Eliab a sak. Apâhni lah Abinadab, apâthum lah Shimea,
14 wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
apali nah Nethanel, apanga nah Raddai,
15 wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
ataruk nah Ozem, asari nah Devit a sak.
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
A tawncanu hai ao teh Zeruiah hoi Abigail heh a tawncanu doeh. Zeruiah casak Abishai, Joab, Asahel hoi kathum touh a pha awh.
17 Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
Abigail ni Amasa a sak. Amasa na pa teh Ishmael Jether doeh.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
Khetsron capa Kaleb ni a yu Azubah hoi Jerioth koehoi ca a sak. Ahnie canaw teh: Jesher, Shobab hoi Ardon.
19 Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
Azubah a due hoi Kaleb ni Epharath hah ama koe a la teh ahni hanlah Hur a sak pouh.
20 Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
Hur ni Uri hah a sak teh Uri ni Bezalel a sak.
21 Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
Hahoi Khetsron ni Gilead tami Makhir canu a ikhai teh, Khetsron hah a la teh kum 60 a pha toteh, Khetsron hanlah Segub a sak pouh.
22 Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
Segub ni Jair a sak teh Gilead ram e khopui 23 touh hah ahnie lah ao.
23 (Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
Hatei, Geshur, Aram khocanaw hoi Jair, hotnaw thung hoi Kenath hoi a khotenaw, khopui 60 touh a la sin. Hotnaw pueng teh Gilead na pa Makhir casaknaw e doeh.
24 Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
Hahoi Khetsron teh Kalebephratha kho dawk a due. Khetsron yu Abijah ni ahni hanlah Tekoa na pa Ashhur a sak pouh.
25 Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
Khetsron e camin Jerahmeel casaknaw a camin Ram hoi Bunah, Oren hoi Ozem hoi Ahijah naw doeh.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
Jerahmeel teh a yu bout a la teh, a min teh Onam manu Atarah doeh.
27 Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
Jerahmeel camin Ram casaknaw teh Maaz, Jamin hoi Eker naw doeh.
28 Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
Onam casak teh Shammai hoi Jada lah ao teh Shammai casak teh Nadab hoi Abishur lah ao.
29 Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
Abishur e yu min teh Abihail doeh, ahni ni Ahban hoi Molid a sak pouh.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
Nadab casak teh Seled hoi Appaimnaw doeh, Seled teh ca sak laipalah a due.
31 Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
Appaim casak teh Ishi, Ishi casak teh Sheshan, Sheshan casak teh Ahlai.
32 Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
Shammai e nawngha Jada casak teh Jether hoi Jonathan lah a o, Jether teh ca sak laipalah a due.
33 Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
Jonathan casak teh Peleth, Zaza. Hetnaw teh, Jerahmeel casak lah ao awh.
34 Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
Sheshan teh ca tongpa awm hoeh, napuinaw dueng doeh kaawm. Sheshan koevah, Izip san, a min lah Jarha ao.
35 Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
Sheshan ni a canu teh a san Jarha koevah a yu lah a poe dawkvah ahni hanlah Attai a sak pouh.
36 Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
Attai ni Nathan a sak teh Nathan ni Zabad a sak.
37 Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
Zabad ni Ephlal a sak teh Ephlal ni Obed a sak.
38 Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
Obed ni Jehu a sak teh Jehu ni Azariah a sak.
39 Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
Azariah ni Helez a sak teh Helez ni Eleasah a sak.
40 Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
Eleasah ni Sismai a sak teh Sismai ni Shallum a sak.
41 Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
Shallum ni Jekamiah a sak teh Jekamiah ni Elishama a sak.
42 Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
Jerahmeel nawngha Kaleb casak Ziph na pa Mesha hah a camin teh Mareshah casak Hebron na pa lah ao.
43 Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
Hebron casak teh Korah, Tappuah, Rekem hoi Shema doeh.
44 Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
Shema ni Jorkeam na pa Raham a sak teh Rekem ni Shammai a sak.
45 Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
Shammai casak Moan doeh, Maon teh Bethzur na pa doeh.
46 Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
Kaleb e ado Ephah ni Haran, Moza hoi Gazez a sak. Haran ni Gazez a sak.
47 Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
Jahdai casak teh Regem, Jotham, Geshan, Pelet, Ephah hoi Shaaph doeh.
48 Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
Kaleb e ado Maakah ni Sheber hoi Tirhannah a sak.
49 Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
Madmannah na pa Shaaph, Makhbena na pa Sheva hoi Gibea na pa hai a sak. Aksah heh Kaleb canu doeh.
50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
Hetnaw heh Kaleb casak lah ao awh. Hur casak a camin lah Epharath lah ao teh, Kiriathjearim na pa Shobal.
51 Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
Bethlehem na pa Salma, Bethgader na pa Hareph hai ao.
52 Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
Kiriathjearim na pa Shobal casak thung hoi Manahati tangawn, Haroehnaw hai ao rah.
53 pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
Kiriathjearim casak dawkvah Ithrite hoi Puthit, Shumati, Mishraitinaw ao awh teh, hetnaw koehoi Zorath hoi Eshtaol lah a tâco.
54 Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
Salma casak Bethlehem, Netophah, Atrothbethjoab hoi Manahati tangawn Zorithnaw hah doeh.
55 pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.
Cakathutkungnaw casak lah kaawm e teh Jabez, Tirathites, Shimeathi hoi Shukathi doeh. Hetnaw heh Rekhab imthung e a na pa Khammath koehoi ka tâcawt e Keninaw doeh.

< 1 Nyakati 2 >