< 1 Nyakati 19 >

1 Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
Después de esto sucedió que la muerte llegó a Nahas, el rey de los hijos de Amón, y su hijo se convirtió en rey en su lugar.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
Y dijo David: Seré amigo de Hanun, el hijo de Nahas, porque su padre era amigo mío. Entonces David le envió hombres para que le dieran palabras de consuelo a causa de su padre. Y los siervos de David fueron a Hanun, a la tierra de los hijos de Amón, ofreciéndole consuelo.
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
Pero los jefes de los hijos de Amón le dijeron a Hanun: ¿Te parece que David está honrando a tu padre, enviando consoladores? ¿No está claro que estos hombres solo han venido para recorrer la tierra y hacer una observación secreta de ella para que puedan vencerla?
4 Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Entonces, Hanun tomó a los sirvientes de David, y cortándose el pelo y las faldas de sus ropas hasta las caderas, dejándolas al descubierto, después los despidió.
5 Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
Entonces ciertos hombres fueron y le dieron a David la noticia de lo que les habían hecho. Y él envió con el propósito de encontrarlos; porque los hombres fueron grandemente avergonzados. Y el rey dijo: Mantente en Jericó hasta que tu cabello vuelva a ser largo, y luego vuelve.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
Y cuando los hijos de Amón vieron que se habían hecho odiosos a David, Hanun y los hijos de Amón enviaron mil talentos de plata como pago por los carros de combate y tropas de caballería de Mesopotamia, Siria, Maaca y Soba.
7 Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
Así que con este dinero tomaron a sueldo treinta y dos mil carros de guerra, y la ayuda del rey de Maaca y su gente, quienes vinieron y tomaron su posición frente a Medeba. Y los hijos de Amón se juntaron de sus pueblos para pelear.
8 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
Y al oírlo David, envió a Joab con todo el ejército de combatientes.
9 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
Entonces los hijos de Amón salieron y pusieron sus fuerzas en posición en el camino hacia la ciudad; y los reyes que habían venido estaban estacionados solos en el campo.
10 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Cuando Joab vio que sus fuerzas estaban en posición contra él delante y detrás de él, tomó a los mejores hombres de Israel y los puso en fila contra los arameos;
11 Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
Y el resto de la gente se puso en posición contra los hijos de Amón con Abisai, su hermano, a la cabeza.
12 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
Y él dijo: Si los arameos son más fuertes y me superan, vengan en mi ayuda; y si los hijos de Amón te superan, acudiré en tu ayuda.
13 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Anímate y seamos fuertes para nuestro pueblo y para los pueblos de nuestro Dios; y que el Señor haga lo que le parezca bien.
14 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Entonces Joab y las personas que estaban con él avanzaron en la lucha contra los sirios, y huyeron éstos ante él.
15 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
Y cuando los hijos de Amón vieron la huida de los sirios, ellos mismos huyeron de Abisai, su hermano, y entraron en la ciudad. Entonces Joab volvió a Jerusalén.
16 Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
Y cuando los sirios vieron que Israel los había vencido, enviaron hombres a buscar a los sirios que estaban al otro lado del río, con Sofac, el capitán del ejército de Hadadezer, a la cabeza.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
Y se le dio a David una palabra de esto; y reunió a todo Israel, pasó por el Jordán y puso sus fuerzas en posición contra ellos. Y cuando las fuerzas de David estaban en posición contra los sirios, se inició la lucha.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
Y los sirios huyeron delante de Israel; y David puso a la espada a los hombres de siete mil carros de guerra arameos y cuarenta mil hombres de infantería, y mató a Sofac, el capitán del ejército.
19 Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Y cuando los siervos de Hadad Ezer vieron que fueron vencidos por Israel, hicieron la paz con David y se convirtieron en sus siervos. Y Los sirios no ayudarían más a los hijos de Amón.

< 1 Nyakati 19 >