< 1 Nyakati 19 >
1 Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
E aconteceu, depois disto, que Nahas, rei dos filhos de Ammon, morreu: e seu filho reinou em seu lugar.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
Então disse David: Usarei de beneficência com Hanun, filho de Nahas, porque seu pai usou de beneficência comigo. Pelo que David enviou mensageiros para o consolarem acerca de seu pai. E, vindo os servos de David à terra dos filhos de Ammon, a Hanun, para o consolarem,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
Disseram os príncipes dos filhos de Ammon a Hanun: Porventura honra David a teu pai aos teus olhos, porque te mandou consoladores? não vieram seus servos a ti, a esquadrinhar, e a transtornar, e a espiar a terra?
4 Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Pelo que Hanun tomou os servos de David, e os rapou, e lhes cortou os vestidos no meio até à coxa da perna, e os despediu.
5 Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
E foram-se, e avisaram a David acerca destes homens, e mandou ao encontro deles; porque aqueles homens estavam sobremaneira envergonhados. Disse pois o rei: deixai-vos ficar em Jericó, até que vos torne a crescer a barba, e então tornai.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
Vendo pois os filhos de Ammon que se tinham feito odiosos para com David, então enviou Hanun, e os filhos de Ammon, mil talentos de prata, para alugarem para si carros e cavaleiros de Mesopotâmia, e da Síria de Maaca, e de Zoba.
7 Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
E alugaram para si trinta e dois mil carros, e o rei de Maaca e a sua gente, e eles vieram, e se acamparam diante de Medeba: também os filhos de Ammon se ajuntaram das suas cidades, e vieram para a guerra.
8 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
O que ouvindo David, enviou Joab e todo o exército dos homens valorosos.
9 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
E, saindo os filhos de Ammon, ordenaram a batalha à porta da cidade: porém os reis que vieram se puseram à parte no campo.
10 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
E, vendo Joab que a frente da batalha estava contra ele por diante e por detraz, fez escolha dentre os mais escolhidos de Israel, e os ordenou contra os siros:
11 Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
E o resto do povo entregou na mão de Abisai, seu irmão; e puseram-se em ordem de batalha contra os filhos de Ammon.
12 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
E disse: Se os siros forem mais fortes do que eu, tu virás socorrer-me; e, se os filhos de Ammon forem mais fortes do que tu, então eu te socorrerei a ti.
13 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Esforça-te, e esforcemo-nos pelo nosso povo, e pelas cidades do nosso Deus, e faça o Senhor o que parecer bem aos seus olhos.
14 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Então se chegou Joab, e o povo que tinha consigo, diante dos siros, para a batalha; e fugiram de diante dele.
15 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
Vendo pois os filhos de Ammon que os siros fugiram, também eles fugiram de diante de Abisai, seu irmão, e entraram na cidade: e veio Joab para Jerusalém.
16 Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
E, vendo os siros que foram derrotados diante de Israel, enviaram mensageiros, e fizeram sair os siros que habitavam da banda de além do rio: e Sophac, capitão do exército de Hadar-ezer, marchava diante deles.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
Do que avisado David, ajuntou a todo o Israel, e passou o Jordão, e veio ter com eles, e ordenou contra eles a batalha: e, tendo David ordenado a batalha contra os siros, pelejaram contra ele.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
Porém os siros fugiram de diante de Israel, e feriu David, dos siros, sete mil cavalos de carros, e quarenta mil homens de pé: e a Sophac, capitão do exército, matou.
19 Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Vendo pois os servos d'Hadar-ezer que tinham sido feridos diante de Israel, fizeram paz com David, e o serviram: e os siros nunca mais quizeram socorrer os filhos de Ammon.