< 1 Nyakati 19 >

1 Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
E aconteceu, depois d'isto, que Nahas, rei dos filhos d'Ammon, morreu: e seu filho reinou em seu logar.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
Então disse David: Usarei de beneficencia com Hanun, filho de Nahas, porque seu pae usou de beneficencia comigo. Pelo que David enviou mensageiros para o consolarem ácerca de seu pae. E, vindo os servos de David á terra dos filhos de Ammon, a Hanun, para o consolarem,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
Disseram os principes dos filhos de Ammon a Hanun: Porventura honra David a teu pae aos teus olhos, porque te mandou consoladores? não vieram seus servos a ti, a esquadrinhar, e a transtornar, e a espiar a terra?
4 Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Pelo que Hanun tomou os servos de David, e os rapou, e lhes cortou os vestidos no meio até á coxa da perna, e os despediu.
5 Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
E foram-se, e avisaram a David ácerca d'estes homens, e mandou ao encontro d'elles; porque aquelles homens estavam sobremaneira envergonhados. Disse pois o rei: Deixae-vos ficar em Jericó, até que vos torne a crescer a barba, e então tornae.
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
Vendo pois os filhos de Ammon que se tinham feito odiosos para com David, então enviou Hanun, e os filhos de Ammon, mil talentos de prata, para alugarem para si carros e cavalleiros de Mesopotamia, e da Syria de Maaca, e de Zoba.
7 Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
E alugaram para si trinta e dois mil carros, e o rei de Maaca e a sua gente, e elles vieram, e se acamparam diante de Medeba: tambem os filhos de Ammon se ajuntaram das suas cidades, e vieram para a guerra.
8 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
O que ouvindo David, enviou Joab e todo o exercito dos homens valorosos.
9 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
E, saindo os filhos d'Ammon, ordenaram a batalha á porta da cidade: porém os reis que vieram se pozeram á parte no campo.
10 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
E, vendo Joab que a frente da batalha estava contra elle por diante e por detraz, fez escolha d'entre os mais escolhidos de Israel, e os ordenou contra os syros:
11 Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
E o resto do povo entregou na mão de Abisai, seu irmão; e pozeram-se em ordem de batalha contra os filhos d'Ammon.
12 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
E disse: Se os syros forem mais fortes do que eu, tu virás soccorrer-me; e, se os filhos de Ammon forem mais fortes do que tu, então eu te soccorrerei a ti.
13 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Esforça-te, e esforcemo-nos pelo nosso povo, e pelas cidades do nosso Deus, e faça o Senhor o que parecer bem aos seus olhos.
14 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Então se chegou Joab, e o povo que tinha comsigo, diante dos syros, para a batalha; e fugiram de diante d'elle.
15 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
Vendo pois os filhos d'Ammon que os syros fugiram, tambem elles fugiram de diante de Abisai, seu irmão, e entraram na cidade: e veiu Joab para Jerusalem.
16 Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
E, vendo os syros que foram derrotados diante d'Israel, enviaram mensageiros, e fizeram sair os syros que habitavam da banda d'além do rio: e Sophac, capitão do exercito de Hadar-ezer, marchava diante d'elles.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
Do que avisado David, ajuntou a todo o Israel, e passou o Jordão, e veiu ter com elles, e ordenou contra elles a batalha: e, tendo David ordenado a batalha contra os syros, pelejaram contra elle.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
Porém os syros fugiram de diante d'Israel, e feriu David, dos syros, sete mil cavallos de carros, e quarenta mil homens de pé: e a Sophac, capitão do exercito, matou.
19 Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Vendo pois os servos d'Hadar-ezer que tinham sido feridos diante d'Israel, fizeram paz com David, e o serviram: e os syros nunca mais quizeram soccorrer os filhos d'Ammon.

< 1 Nyakati 19 >