< 1 Nyakati 19 >

1 Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
Après cela, Naas, roi des fils d'Ammon, mourut, et son fils régna à sa place.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
David dit: " Je montrerai de la bienveillance à Hanon, fils de Naas, car son père m'a montré de la bienveillance. " Et David envoya des messagers pour le consoler au sujet de son père. Lorsque les serviteurs de David furent arrivés, dans le pays des fils d'Ammon, auprès de Hanon, pour le consoler,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
les princes des fils d'Ammon dirent à Hanon: " Penses-tu que ce soit pour honorer ton père que David t'envoie des consolateurs? N'est-ce pas pour reconnaître et détruire, et pour explorer le pays, que ses serviteurs sont venus vers toi! "
4 Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Alors Hanon, ayant saisi les serviteurs de David, les rasa et coupa leurs habits à mi-hauteur, jusqu'à la hanche, et il les renvoya.
5 Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
On alla informer David de ce qui était arrivé à ses hommes, et il envoya des gens à leur rencontre, car ces hommes étaient dans une grande confusion, et le roi leur fit dire: " Restez à Jéricho, jusqu'à ce que votre barbe ait repoussé, et vous reviendrez ensuite. "
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
Les fils d'Ammon virent qu'ils s'étaient rendus odieux à David, et Hanon et les fils d'Ammon envoyèrent mille talents d'argent pour prendre à leur solde des chars et des cavaliers chez les Syriens de Mésopotamie et chez les Syriens de Maacha et de Soba.
7 Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
Ils prirent à leur solde trente-deux mille chars, et le roi de Maacha avec son peuple, lesquels vinrent camper près de Médaba. Les fils d'Ammon se rassemblèrent de leurs villes et vinrent au combat.
8 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
David l'apprit et fit partir contre eux Joab et toute l'armée, les hommes vaillants.
9 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
Les fils d'Ammon sortirent et se rangèrent en bataille à la porte de la ville; les rois qui étaient venus étaient à part dans la campagne.
10 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Lorsque Joab vit qu'il y avait un front de bataille devant et derrière lui, il choisit parmi toute l'élite d'Israël un corps qu'il rangea en face des Syriens,
11 Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
et il mit le reste du peuple sous le commandement de son frère Abisaï, les rangeant en face des fils d'Ammon. Il dit:
12 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
" Si les Syriens sont plus forts que moi, tu viendras à mon secours; et si les fils d'Ammon sont plus forts que toi, je te secourrai.
13 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Sois ferme, et combattons vaillamment pour notre peuple et pour les villes de notre Dieu, et que Yahweh fasse ce qui semblera bon à ses yeux! "
14 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Joab s'avança donc, ainsi que le peuple qui était avec lui, contre les Syriens pour les attaquer, et ceux-ci s'enfuirent devant lui.
15 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
Les fils d'Ammon, voyant que les Syriens avaient pris la fuite, s'enfuirent, eux aussi, devant Abisaï, frère de Joab, et rentrèrent dans la ville. Et Joab rentra dans Jérusalem.
16 Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
Les Syriens, voyant qu'ils avaient été battus devant Israël, envoyèrent des messagers pour faire venir les Syriens qui étaient de l'autre côté du fleuve; et Sophach, chef de l'armée d'Hadarézer marchait devant eux.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
David en reçut la nouvelle et, ayant assemblé tout Israël, il passa le Jourdain, vint vers eux, et disposa l'attaque contre eux; et David rangea son armée en bataille contre les Syriens. Ceux-ci engagèrent le combat contre lui,
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
mais les Syriens s'enfuirent devant Israël, et David tua aux Syriens les chevaux de sept mille chars et quarante mille hommes de pied; il mit aussi à mort Sophach, chef de l'armée.
19 Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Les vassaux d'Hadarézer, se voyant battus devant Israël, firent la paix avec David et lui furent assujettis. Et les Syriens ne voulurent plus porter secours aux fils d'Ammon.

< 1 Nyakati 19 >