< 1 Nyakati 19 >

1 Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
Nogen Tid efter døde Ammoniternes Konge Nahasj, og hans Søn Hanun blev Konge i hans Sted.
2 Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
Da tænkte David: "Jeg vil vise Hanun, Nahasj's Søn, Venlighed, thi hans Fader viste mig Venlighed." Og David sendte Folk for at vise ham Deltagelse i Anledning at hans Faders Død. Men da Davids Mænd kom til Ammoniteroes Land til Hanun for at vise ham Deltagelse,
3 wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
sagde Ammoniternes Høvdinger til Hanun: "Tror du virkelig, det er for at hædre din Fader, at David sender Bud og viser dig Deltagelse? Mon ikke det er for at udforske og ødelægge Landet og udspejde det, at hans Folk kommer til dig?"
4 Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
Da tog Hanun Davids Folk og lod dem rage og Halvdelen af deres Klæder skære af til Skridtet, og derpå lod han dem gå.
5 Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
Da David fik Efterretning om Mændenes Behandling, sendte han dem et Bud i Møde; thi Mændene var blevet grovelig forhånet; og Kongen lod sige: "Bliv i Jeriko, til eders Skæg er vokset ud!"
6 Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
Men da Ammoniterne så, at de havde lagt sig for Had hos David, sendte Hanun og Ammoniterne 1000 Talenter Sølv for at leje Vogne og Ryttere i Aram-Naharajim, Aram Ma'aka og Zoba;
7 Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
og de lejede 32000 Vogne og Kongen af Ma'aka med hans Folk, og de kom og slog Lejr uden for Medeba; imidlertid havde Ammoniterne samlet sig fra deres Byer og rykkede ud til Kamp.
8 Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
Da David hørte det, sendte han Joab af Sted med hele Hæren og Kærnetropperne.
9 Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
Ammoniterne rykkede så ud og stillede sig op til Kamp ved Byens Port, medens Kongerne, der var kommet til, stod for sig selv på åben Mark.
10 Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
Da Joab så, at Angreb truede ham både forfra og bagfra, gjorde han et Udvalg blandt alt Israels udsøgte Mandskab og tog Stilling over for Aramæerne,
11 Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
medens han overlod Resten af Mandskabet til sin Broder Absjaj, og de tog Stilling over for Ammoniterne.
12 Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
Og han sagde: "Hvis Aramæerne bliver mig for stærke, skal du ile mig til Hjælp; men bliver Ammoniterne dig for stærke, skal jeg hjælpe dig.
13 Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
Tag Mod til dig og lad os tappert værge vort Folk og vor Guds Byer - så får HERREN gøre, hvad ham tykkes godt!"
14 Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
Derpå rykkede Joab frem med sine Folk til Kamp mod Aramæerne, og de flygtede for ham.
15 Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
Og da Ammoniterne så, at Aramæerne tog Flugten, flygtede også de forhans Broder Absjaj og trak sig ind i Byen. Derpå kom Joab til Jerusalem.
16 Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
Men da Aramæerne så, at de var slået af Israel, sendte de Bud og fik Aramæerne hinsides Floden til at rykke ud med Sjofak, Hadar'ezers Hærfører, i Spidsen.
17 Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
Da David fik Efterretning herom, samlede han hele Israel, satte over Jordan og kom til Helam, hvor David stillede sig op til Kamp mod Aramæerne, og de angreb ham.
18 Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
Men Aramæerne flygtede for Israel, og David nedhuggede 7.000 Stridsheste og 40.000 Mand Fodfolk af Aram; også Hærføreren Sjofak huggede han ned.
19 Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Da alle Hadar'ezers Lydkonger så, at de var slået af Israel, sluttede de Fred med David og underkastede sig, og Aramæerne vilde ikke hjælpe Ammoniterne mere.

< 1 Nyakati 19 >