< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
Bir süre sonra, Davut Filistliler'i yenip boyunduruğu altına aldı; Gat'ı ve çevresindeki köyleri Filistliler'in yönetiminden çıkardı.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
Moavlılar'ı da bozguna uğrattı. Onlar Davut'un haraç ödeyen köleleri oldular.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
Davut Fırat'a kadar krallığını pekiştirmeye giden Sova Kralı Hadadezer'i de Hama yakınlarında yendi.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
Bin savaş arabasını, yedi bin atlısını, yirmi bin yaya askerini ele geçirdi. Yüz savaş arabası için gereken atların dışındaki bütün atları da sakatladı.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Sova Kralı Hadadezer'e yardıma gelen Şam Aramlıları'ndan yirmi iki bin kişiyi öldürdü.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Sonra Şam Aramlıları'nın ülkesine askeri birlikler yerleştirdi. Onlar da Davut'un haraç ödeyen köleleri oldular. RAB Davut'u gittiği her yerde zafere ulaştırdı.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Davut Hadadezer'in komutanlarının taşıdığı altın kalkanları alıp Yeruşalim'e götürdü.
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
Ayrıca Hadadezer'in yönetimindeki Tivhat ve Kun kentlerinden bol miktarda tunç aldı. Süleyman bunu havuz, sütunlar ve çeşitli eşyalar yapmak için kullandı.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
Hama Kralı Tou, Davut'un Sova Kralı Hadadezer'in bütün ordusunu bozguna uğrattığını duydu.
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
Tou Kral Davut'u selamlamak ve Hadadezer'le savaşıp yendiği için kutlamak üzere oğlu Hadoram'ı ona gönderdi. Çünkü Tou Hadadezer'le sürekli savaşmıştı. Hadoram Davut'a her türlü altın, gümüş, tunç armağanlar getirdi.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
Kral Davut bu armağanları bütün uluslardan –Edom, Moav, Ammonlular, Filistliler ve Amalekliler'den– ele geçirdiği altın ve gümüşle birlikte RAB'be adadı.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Seruya oğlu Avişay Tuz Vadisi'nde on sekiz bin Edomlu öldürdü.
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
Edom'a askeri birlikler yerleştirdi. Edomlular'ın tümü Davut'un köleleri oldular. RAB Davut'u gittiği her yerde zafere ulaştırdı.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Bütün İsrail'de krallık yapan Davut halkına doğruluk ve adalet sağladı.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Seruya oğlu Yoav ordu komutanı, Ahilut oğlu Yehoşafat devlet tarihçisiydi.
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
Ahituv oğlu Sadok'la Aviyatar oğlu Ahimelek kâhin, Şavşa yazmandı.
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
Yehoyada oğlu Benaya Keretliler'le Peletliler'in komutanıydı. Davut'un oğulları da sarayda yüksek görevlere atanmışlardı.

< 1 Nyakati 18 >