< 1 Nyakati 18 >
1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
Derefter slog David de Philisteer, och undertryckte dem, och tog Gath och dess döttrar utu de Philisteers hand.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
Slog han ock de Moabiter, så att de Moabiter vordo David underdånige, och förde honom skänker.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
Han slog ock HadarEser, Konungen i Zoba, uti Hamath, då han dit drog, till att uppresa sitt tecken vid den älfvena Phrath.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
Och David vann af honom tusende vagnar, sjutusend resenärar, och tjugutusend män till fots och David hasade alla vagnhästarna, och behöll hundrade vagnar qvara.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Och de Syrer af Damasco kommo HadarEser, Konungenom i Zoba, till hjelp; men David slog de samma Syrer, tu och tjugu tusend män;
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Och lade folk till Damascon i Syrien, så att de Syrer vordo David underdånige, och förde honom skänker; ty Herren halp David, ehvart han for.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Och David tog de gyldene sköldar, som HadarEsers tjenare hade, och förde dem till Jerusalem.
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
Tog också David utu HadarEsers städer, Tibhath och Chun, ganska mycken koppar, af hvilkom Salomo kopparhafvet, och stoderna och kopparkärilen gjorde.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
Och då Thou, Konungen i Hamath, hörde, att David hade slagit alla HadarEsers magt, Konungens i Zoba;
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
Sände han sin son Hadoram till Konung David, och lät helsa och välsigna honom, att han med HadarEser stridt, och honom slagit hade; ty Thou hade örlig med HadarEser. Och all gyldene, silfver, och kopparkärile,
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
Dem helgade Konung David Herranom, med det silfver och guld, som han tagit hade ifrå Hedningarna, nämliga ifrå de Edomeer, Moabiter, Ammoniter, Philisteer och Amalekiter.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Och Abisai, ZeruJa son, slog de Edomeer i saltdalenom, adertontusend;
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
Och lade folk i Edomeen; så att alle Edomeer voro David underdånige; ty Herren halp David, ehvart han drog.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Alltså regerade David öfver hela Israel, och höll rätt och rättvisa allo sino folke.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Joab, ZeruJa son, var öfver hären; Jojaphat, Ahiluds son, var canceller.
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
Zadok, Ahitobs son, och AbiMelech, AbJathars son, voro Prester; Sausa var skrifvare.
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
Benaja, Jojada son, var öfver Crethi och Plethi; och de förste Davids söner voro Konungenom vid handen.