< 1 Nyakati 18 >
1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
Derefter slo David filistrene og ydmyket dem, og han tok Gat med tilhørende småbyer ut av filistrenes hender.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
Han slo også moabittene, og moabittene blev Davids tjenere og måtte svare ham skatt.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
Likeledes slo David kongen i Soba Hadareser ved Hamat, da han drog avsted for å styrke sitt herredømme ved Frat-elven.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
Og David tok fra ham tusen vognhester og syv tusen hestfolk og tyve tusen mann fotfolk; og David lot skjære fotsenene over på alle vognhestene; bare hundre vognhester sparte han.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Syrerne fra Damaskus kom for å hjelpe Hadareser, kongen i Soba; men David slo to og tyve tusen mann av dem.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Og David la krigsmannskap i det damaskenske Syria, og syrerne blev Davids tjenere og måtte svare ham skatt. Således hjalp Herren David overalt hvor han drog frem.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
David tok de gullskjold som Hadaresers tjenere hadde båret, og førte dem til Jerusalem.
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
Og fra Hadaresers byer Tibhat og Kun tok David en stor mengde kobber; av det gjorde Salomo kobberhavet og søilene og kobberkarene.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
Da kongen i Hamat To'u hørte at David hadde slått hele Soba-kongen Hadaresers hær,
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
sendte han sin sønn Hadoram til kong David for å hilse på ham og ønske ham til lykke, fordi han hadde stridt mot Hadareser og slått ham; for Hadareser hadde jevnlig ført krig mot To'u. Han sendte også alle slags gullkar og sølvkar og kobberkar.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
Også dem helliget kong David til Herren sammen med det sølv og gull han hadde tatt fra alle hedningefolkene: fra Edom og fra Moab og fra Ammons barn og fra filistrene og fra amalekittene.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Det var Absai, Serujas sønn, som slo edomittene i Saltdalen, atten tusen mann.
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
Så la han krigsmannskap i Edom, og alle edomittene blev Davids tjenere. Således hjalp Herren David overalt hvor han drog frem.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Så regjerte nu David over hele Israel, og han gjorde rett og rettferdighet mot hele sitt folk.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Joab, Serujas sønn, var høvding over hæren, og Josafat, Akiluds sønn, historieskriver;
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
Sadok, Akitubs sønn, og Abimelek, Ebjatars sønn, var prester og Savsa statsskriver;
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
Benaja, Jojadas sønn, var høvding over livvakten, og Davids sønner var de første ved kongens side.