< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
And it came to pass afterwards, that David struck the Philistines, and routed them, and took Geth and its villages out of the hand of the Philistines.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
And he struck Moab; and the Moabites became servants to David, [and] tributaries.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
And David struck Adraazar king of Suba of Emath, as he was going to establish power toward the river Euphrates.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
And David took of them a thousand chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand infantry: and David houghed all the chariot [horses], but there were reserved of them a hundred chariots.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
And the Syrian came from Damascus to help Adraazar king of Suba; and David struck of the Syrian [army] twenty and two thousand men.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
And David put a garrison in Syria near Damascus; and they became tributary servants to David: and the Lord delivered David wherever he went.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
And David took the golden collars that were on the servants of Adraazar, and brought them to Jerusalem.
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
And David took out of Matabeth, and out of the chief cities of Adraazar very much brass: of this Solomon made the brazen sea, and the pillars, and the brazen vessels.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
And Thoa king of Emath heard that David had struck the whole force of Adraazar king of Suba.
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
And he sent Aduram his son to king David to ask how he was, and to congratulate him because he had fought against Adraazar, and struck him; for Thoa was the enemy of Adraazar.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
And all the golden and silver and brazen vessels, even these king David consecrated to the Lord, with the silver and the gold which he took from all the nations; from Idumaea, and Moab, and from the children of Ammon, and from the Philistines, and from Amalec.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
And Abesa son of Saruia struck the Idumeans in the valley of Salt, eighteen thousand.
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
And he put garrisons in the valley; and all the Idumaeans became David's servants: and the Lord delivered David wherever he went.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
So David reigned over all Israel; and he executed judgment and justice to all his people.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
And Joab the son of Saruia [was] over the army, and Josaphat the son of Achilud [was] recorder.
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
And Sadoc son of Achitob, and Achimelech son of Abiathar, [were] the priests; and Susa [was] the scribe;
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
and Banaeas the son of Jodae [was] over the Cherethite and the Phelethite, and the sons of David were the chief deputies of the king.

< 1 Nyakati 18 >