< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
Nogen Tid efter slog David Filisterne og undertvang dem, og han fratog Filisterne Gat med Småbyer.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
Fremdeles slog han Moabiterne; og Moabiterne blev Davids skatskyldige Undersåtter.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
Ligeledes slog David Kong Hadar'ezer af Zoba i Nærheden af Hamat, da han var draget ud for at underlægge sig Egnene ved Eufratfloden.
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
David fratog ham 1.000 Vogne, 7.008 Ryttere og 20.000 Mand Fodfolk og lod alle Hestene lamme på hundrede nær, som han skånede.
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Og da Aramæerne fra Darmaskus kom Kong Hadar'ezer af Zoba til Hjælp, slog David 22.000 Mand af Aramæerne.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Derpå indsatte David Fogeder i det darmaskenske Aram, og Aramæerne blev Davids skatskyldige Undersåtter. Således gav HERREN David Sejr, overalt hvor han drog frem.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Og David tog de Guldskjolde, Hadar'ezers Folk havde båret, og bragte dem til Jerusalem;
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
og fra Hadar'ezers Byer, Tibhat og Kun, bortførte David Kobber i store Mængder; deraf lod Salomo Kobberhavet, Søjlerne og Kobbersagerne lave.
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
Men da Kong To'u af Hamat hørte, at David havde slået hele Kong Hadar'ezer af Zobas Stridsmagt,
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
sendte han sin Søn Hadoram til Kong David for at hilse på ham og lykønske ham til, at han havde kæmpet med Hadar'ezer og slået ham - Hadar'ezer havde nemlig ligget i Krig med To'u - og han medbragte alle Hånde Sølv-, Guld og Kobbersager.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
Også dem helligede Kong David HERREN tillige med det Sølv og Guld, han havde taget fra alle Folkeslagene, Edom, Moab, Ammoniterne, Filisterne og Amalek.
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Og Absjaj, Zerujas Søn, slog Edom i Saltdalen, 18000 Mand;
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
derpå indsatte han Fogeder i Edom, og alle Edomiterne blev Davids Undersåtter. Således gav HERREN David Sejr, overalt hvor han drog frem.
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Og David var Konge over hele Israel, og han øvede Ret og Retfærdighed mod hele sit Folk.
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Joab, Zerujas Søn, var sat over Hæren; Josjafat, Ahiluds Søn, var Kansler;
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
Zadok, Ahitubs Søn, og Abimelek, Ebjatars Søn, var Præster; Sjavsja var Statsskriver;
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
Benaja, Jojadas Søn, var sat over Kreterne og Pleterne, og Davids Sønner var de ypperste ved Kongens Side.

< 1 Nyakati 18 >