< 1 Nyakati 18 >
1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
[達味的武功]此後,達味攻打培肋舍特人,將他們克服,由培肋舍特人手中,奪取了加特城及所屬村鎮。
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
以後打敗了摩阿布,摩阿布人也臣屬於達味,給他進貢。
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
當祚巴哈瑪特王哈達德則爾向幼發拉的河伸展自己的勢力時,達味也打敗了他,
4 Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
擄獲了他的車輛一千,騎兵七千,步兵兩萬;達味割斷了所有拉戰車的馬蹄筋,只留下足以拉一百輛車的馬。
5 Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
後有大馬士革的阿蘭人,來援助祚巴王哈達德則爾,達味擊殺了兩萬二千阿蘭人。
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
達味遂在大馬士革阿蘭屯兵駐守,阿蘭也臣屬於達味,給他進貢;達味無論往那裏去,上主總使他獲勝。
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
達味奪了哈達德則爾臣僕所帶的金盾牌,送到耶路撒冷。
8 Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
達味又由貝塔和貢,哈達德則爾的兩座城內,奪取了大量的銅;以後撒羅滿用來作銅海、圓柱及銅器。
9 Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
哈瑪特王托烏,聽說達味打敗了祚巴王哈達德則爾所有的軍隊,
10 akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
便派自己的兒子哈多蘭到達味王那裏向他致敬,祝賀他打敗了哈達德則爾,因哈達德則爾原是托烏的敵人;他還送來了各種金、銀、銅器。
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
達味王也將這些,連同那些由各民族,即厄東、摩阿布、阿孟子民、培肋舍特人、阿瑪肋克人所得來的金銀,一起奉獻給上主。
12 Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
責魯雅的兒子阿彼瑟在鹽谷擊殺了一萬八千厄東人後,
13 Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
達味遂又屯兵厄東,厄東人全臣屬於達味。達味無論往那裏去,上主總使他獲勝。[重要的朝臣]
14 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
達味作了全以色列的君王,對自己所有的人民秉公行義。
15 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
責魯雅的兒子約阿布統領軍隊,阿希路得的兒子約沙法特為御史,
16 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
阿希托布的兒子匝多克和厄貝雅塔爾的兒子阿希默肋客任司祭,沙委沙為秘書,
17 naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.
約雅達的兒子貝納雅管理革勒提與培肋提人,達味的兒子們在君王左右為輔相。