< 1 Nyakati 17 >
1 Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”
И бысть егда обиташе Давид в дому своем, и рече Давид к Нафану пророку: се, аз живу в дому кедрове, кивот же завета Господня под кожами.
2 Nathani akamjibu Daudi, “Lolote ulilo nalo moyoni mwako litende, kwa maana Mungu yu pamoja nawe.”
И рече Нафан к Давиду: все еже в сердцы твоем твори, яко Бог с тобою есть.
3 Usiku ule neno la Mungu likamjia Nathani, kusema:
И бысть нощи тоя, и бысть слово Господне к Нафану, глаголя:
4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Wewe hutanijengea mimi nyumba ili nikae humo.
иди и рцы Давиду рабу Моему: сия рече Господь: не созиждеши ты Мне дому, еже обитати Ми в нем:
5 Mimi sijakaa ndani ya nyumba tangu siku ile niliyowatoa Israeli kutoka Misri mpaka leo. Nimehama kutoka hema moja hadi jingine na kutoka mahali pamoja hadi pengine.
яко не обитах в дому от дне, в оньже изведох Израиля (от земли Египетския), даже до дне сего, но бых в скинии и в шатре:
6 Je, popote nilipokwenda pamoja na Waisraeli wote, wakati wowote nilimwambia kiongozi yeyote niliyemwagiza kuwachunga watu wangu, kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?’
во всех аможе ходих со всем Израилем, аще глаголя глаголах коему колену Израилеву, имже повелех да пасут люди Моя, глаголя: чесо ради не создасте Мне дому кедрова?
7 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikuchukua machungani na kutoka kuandama kondoo ili uwatawale watu wangu Israeli.
И ныне тако рцы рабу Моему Давиду: сия рече Господь Вседержитель: Аз изях тя от паствы, егда последовал еси стаду, еже быти тебе вождем над людьми Моими Израилем,
8 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
и бых с тобою во всех, идеже ходил еси, и потребих вся враги твоя от лица твоего, и сотворих тебе имя якоже имя великих, иже на земли:
9 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali na nitawapa ili wawe na mahali pao wenyewe pa kuishi na wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
и дах место людем Моим Израилю, и насадих я, и обитают в нем, и не возскорбят ктому: ни сынове беззакония приложат смирити их якоже от начала
10 na ambavyo wamefanya siku zote tangu nilipowachagua viongozi kwa ajili ya watu wangu Israeli. Pia nitawatiisha adui zenu wote. “‘Pamoja na hayo ninakuambia kwamba Bwana atakujengea nyumba:
и от дний, в няже дах судии людем Моим Израилю, и смирих вся враги твоя, и возращу тя, и дом созиждет ти Господь:
11 Wakati wako utakapokuwa umekwisha, nawe ukawa umekwenda kukaa na baba zako, nitamwinua mzao wako aingie mahali pako kuwa mfalme, mmoja wa wana wako mwenyewe, nami nitaufanya imara ufalme wake.
и будет егда исполнятся дние твои и почиеши со отцы твоими, и воздвигну семя твое по тебе, еже будет от чрева твоего, и возставлю царство его:
12 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili yangu, nami nitakifanya imara kiti cha ufalme wake milele.
той созиждет Мне дом, и укреплю престол его даже до века:
13 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Kamwe sitaondoa upendo wangu kwake, kama nilivyouondoa kwa yeye aliyekutangulia.
Аз буду ему во отца, и той будет Мне в сына: и милость Мою не отиму от него, якоже отях от бывших прежде тебе:
14 Nitamweka juu ya nyumba yangu na ufalme wangu milele; kiti chake cha enzi nitakifanya imara milele.’”
и уверю его в дому Моем и во царствии его даже до века, и престол его будет исправлен до века.
15 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
По всем словесем сим и по всему видению сему тако глаголал есть Нафан к Давиду.
16 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Mimi ni nani, Ee Bwana Mungu, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
И прииде царь Давид, и седе пред Господем, и рече: кто есмь аз, Господи Боже мой? И что дом мой, яко возлюбил мя еси до века?
17 Kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Mungu, umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Umeniangalia kama mtu aliyetukuka kuliko watu wote, Ee Bwana Mungu.
И сия мала суть пред Тобою, Боже, и глаголал еси на дом раба Твоего (еще) издалеча, и призрел еси на мя яко видение человека, и возвысил мя еси, Господи Боже:
18 “Daudi aweza kukuambia nini zaidi kuhusu kumheshimu mtumishi wako? Kwa maana wewe unamjua mtumishi wako,
что приложит еще Давид к Тебе еже прославити? И ты раба Твоего веси:
19 Ee Bwana Mungu. Kwa ajili ya mtumishi wako, tena sawasawa na mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa sana na kujulisha ahadi hizi zote zilizo kubwa sana.
Господи, раба Твоего ради сотворил еси все величие сие и по сердцу Твоему, еже знаема сотворити вся величия Твоя:
20 “Hakuna aliye kama wewe, Ee Bwana Mungu, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe.
Господи, несть подобен Тебе, и несть Бога разве Тебе, по всем елика слышахом ушима нашима,
21 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli: taifa pekee duniani ambalo Mungu wake alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe na kujifanyia jina kwa ajili yake mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
и несть, якоже людие Твои Израиль, язык еще на земли, яко пойде Бог избавити люди Себе, еже положити имя Себе велие и славное, еже изгнати от лица людий Твоих, ихже избавил еси от Египта, языки:
22 Uliwafanya watu wako Israeli kuwa watu wako wewe mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana Mungu, umekuwa Mungu wao.
и дал еси люди Твоя Израиля Тебе в люди даже до века, и Ты, Господи, был еси им в Бога:
23 “Sasa basi, Bwana ahadi uliyoweka kuhusu mtumishi wako na nyumba yake na uithibitishe milele. Fanya kama ulivyoahidi,
и ныне, Господи, слово Твое, еже глаголал еси рабу Твоему и на дом его, да уверится до века: и сотвори якоже глаголал еси,
24 ili ithibitike na jina lako litakuwa kuu milele. Kisha watu watasema, ‘Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu aliye juu ya Israeli, ndiye Mungu wa Israeli.’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itafanywa imara mbele zako.
и да уверится и возвеличится имя Твое даже до века, глаголющих: Господи, Господи Вседержителю, Боже Израилев, и дом Давида раба Твоего да будет исправлен пред Тобою:
25 “Wewe, Mungu wangu, umemfunulia mtumishi wako Daudi kwamba utamjengea yeye nyumba. Hivyo mtumishi wako amekuwa na ujasiri wa kukuomba maombi haya.
Ты бо, Господи Боже мой, отверзл еси ухо раба Твоего создати ему дом, сего ради обрете раб Твой (дерзновение) молитися пред лицем Твоим:
26 Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu! Umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
и ныне, Господи, Ты еси Сам Бог, и глаголал еси к рабу Твоему благая сия:
27 Basi imekupendeza kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu milele machoni pako; kwa ajili yako, Ee Bwana, umeibariki, nayo itabarikiwa milele.”
и ныне начни благословити дом раба Твоего, да будет во веки пред Тобою: яко Ты, Господи, благословил еси, и благослови во веки.